MKUU WA MKOA WA TABORA AHIMIZA WANANCHI KUWAFICHUA WAGENI KWENYE ZOEZI LA USAJILI VITAMBULISHO VYA TAIFA

 
Mkuu wa mkoa wa Tabora Mhe. Agrey Mwandri akiongea na wananchi wa kijiji cha Ussoke Mlimani kushiriki zoezi la usajili wa Vitambulisho vya Taifa. Kushoto ni Maafisa wa NIDA Emiliana Temu na Grace Msacky.


Mwenyekiti wa kijiji cha Ussoke Kilimani Bw. Jackson Kitwe (kushoto/mwenye kofia) Akitoa maelezo kwa Mkuu wa Mkoa Mhe. Agrey Mwandri na Mkuu wa Wilaya ya Urambo Mhe. Anjelina George Kwingwa walipofanya ziara kijijini hapo.  
  Afisa Usajili mkoa wa Tabora Bi Grace Msacky akiwa na Mkuu wa Mkoa Mhe. Agrey Mwandri wakihamasisha wananchi kujitokeza kwa wingi wakati wa zoezi la Usajili linaloendelea Wilayani humo.
 
 Wananchi wa kata ya Mpela wakiwa wamekusanyika kwenye ofisi za Kata ili kuhojiwa na Maafisa uhamiaji ikiwa ni sehemu ya kukamilisha Usajili Vitambulisho vya Taifa unaoendelea Wilayani humo.

Maelekezo hayo ameyatoa wakati alipofanya ziara ya kutembelea maendeleo ya zoezi la Usajili unaoendelea Wilaya ya Urambo kijiji cha Ussoke Kilimani.
“wananchi ndio mnaokaa na hawa watu; mnaifahamu vizuri historia yao na ujaji waoo kwenye maeneo yenu; msikae kimya na kuwaruhusu kujipenyeza kwenye hizi zoezi; tafadhali muisaidie Serikali” alihimiza.
Akimkaribisha Mkuu wa Mkoa huo kuzungumza na wananchi; Mkuu wa Wilaya ya Urambo Mhe. Anjelina Kwinga amesema zoezi la NIDA halina lengo la kuwabagua wananchi isipokuwa kila mtu anayeishi Wilayani humo atapata fursa ya kusajiliwa na kupata Kitambulisho kulingana na hadhi yake (Raia, Mgeni Mkaazi au Mkimbizi).
Aidha amewataka viongozi wote wa Kata na Vijiji kutoa ushirikiano kwa NIDA na kuwasaidia wananchi kusajiliwa pindi zoezi linapofika kwenye maeneo yao.


RC TABORA: TUMIENI FEDHA ZENU ZA MAUZO YA MAZAO KUJILETEA MAENDELEO NA SIO STAREHE NA TIGANYA VINCENT

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 


CKHT SAIDIENI KATIKA UJENZI WA TANZANIA YA VIWANDA-WAZIRI MKUU MSTAAFU

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

ELIMU KWA WAFUGAJI WA NYUKI KUMEONGEZA UZALISHAJI WA ASALI HAPA NCHINI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

WAZIRI NCHEMBA: VITAMBULISHO VYA TAIFA VITAONDOA MAPINGAMIZI YA URAIA KATIKA CHAGUZI

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
 Na Tiganya Vincent-rs Tabora
Vitambulisho wa uraia vitasaidia kuwa na utambuzi wa wananchi utakao ondoa ile tabia ya baadhi ya watu kutilia mashaka wakati wa shughuli mbalimbali ikiwemo kipindi kushiriki katika zoezi la uchaguzi wote wote.

Kauli hiyo ilitolewa jana mjini Tabora na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Dkt.Mwigulu Nchemba wakati uzinduzi wa zoezi la usajili wananchi kwa ajili ya vitambulisho vya kitaifa mkoani humo.

Alisema kuwa mara nyingi mtu anapogombea nafasi yoyote hapa nchini au kunapokuwepo na migogoro ya kugombania mashamba ndio suala la kusema kuwa huyo sio raia linapojitokeza.

Dkt. Nchemba alisema wananchi wenye sifa kuchangamkia zoezi la usajili na upataji wa vitambulisho vya uraia ili kuepuka matatizo kama vile migogoro ikiwemo ya mapingamizi wakati chaguzi mbalimbali na kuiweza Serikali kupanga mipango mbalimbali ya maendeleo kwa ajili ya wananchi wake


Alisema kuwa hata uchumi wa kisasa unaanza na kutambua kwa Serikali kutambua watu iliyonao na ndipo ipange mipango ya maendeleo kwa ajili yao.Waziri huyo aliongeza kuwa hata kwenye vyombo vya fedha kama vile Benki zimekuwa zikiweka riba kubwa katika mikopo kwa sababu ya baadhi wananchi kukosa utambulizi

Naye Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) Andrew Massawe alisema jitihada hizi zote zimelenga kusaidia Serikali na wananchi kutambulika na hatimaye Mashirika, Taasisi na Makampuni nchini kutumia mfumo huu kutoa huduma zenye ubora na tija kwa Taifa.

Alisema mfumo huu una faida nyingi kwa Taifa na mwananchi mmoja mmoja kama vile kuimarisha Ulinzi na Usalama wa nchi, wananchi kutambulika kwa haraka pindi wanapofika kupata huduma za afya na Elimu.

Massawe alisema kuwa faida nyingine ni kurahisisha utambuzi wa makundi yenye mahitaji maalumu ikiwemo utambuzi wa kaya masikini unaofanywa na Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) na upatikanaji wa huduma za kifedha na Simu kirahisi.

Kwa upande wa Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tabora Queen Mlozi aliwaagiza viongozi wa ngazi zote mkoani humo kuhakikisha kuwa anayesajiliwa na kupata kitambulisho cha uraia ni yule mwenye sifa na sio mgeni.

Alisema Serikali ya Mkoa wa Tabora haitasita kumchukulua mtu yoyote atayeshiriki katika udanganyifu utaosababu watu wasio raia kupata vitambulisho vya uraia.

Queen alisema kuwa kila mmoja ni vema akasimama katika nafasi yake kuhakikisha kuwa anafanya kazi kwa umakini na uadilifu wa hali ya juu ili kuleta ufanisi.

Alitoa wito kwa jamii kusaidia kuwafichua watu wasio raia wanaotaka kujipenya ili wapate vitambulisho vya uraia

WALIMU WENYE MADAI HALALI WATAKIWA KUWASILISHA VIELELEZO VYA MADENI YAO KWA MAOFISA ELIMU WAO.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

CCM TABORA YAWATAKA WANAFUNZI KUTOONA UPANDAJI MITI NI ADHABU BALI NI AKIBA KWAO.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa