NA TIGANYA VINCENT
RS TABORA
26 February 2018
WAZIRI
 Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mkuu wa Chuo Kikuu 
Huria cha Tanzania(CKHT) Mizengo Pinda ametoa wito kwa Wataalamu wa Chuo
 hicho kutoa mafunzo  ambayo yatawasaidia wananchi kuleta mageuzi ambayo yatawezesha katika ujenzi wa Tanzania ya Viwanda na hivyo kutimiza  lengo la Serikali ya Awamu ya Tano.
Mkuu huyo wa Chuo Kikuu hicho alitoa kauli hiyo mjini hapa wakati akizungumza na Watumishi na Wanachuo wa CKHT  Tawi la Tabora wakati wa ziara ya siku moja chuoni hapo.
Alisema
 kuwa Chuo hicho kinayo nafasi kubwa ya kuleta mageuzi yatakawawezesha 
wananchi wengi waweze kutoa mchango wao katika ujenzi wa uchumi wa 
viwanda hapa nchini na hivyo kusaidia katika mapambana dhidi ya 
umaskini.
Mkuu
 huyo wa Chuo hicho alisema kuwa hiyo itawezekana ikiwa elimu 
itakayotolewa itakuwa ikisaidia katika kujibu matatizo ya wananchi kwa 
kuwa na wahitimu ambao wanaweze kuwa mfano kwa wananchi ili waweze 
kujifunza kwao mbinu zitakazowawezesha kujiletea maendeleo.
Aidha
 Waziri Mkuu huyo Mstaafu aliwataka Watendaji na wadau mbalimbali 
kusaidia kuwahamasisha walimu wengi hasa wa shule za Msingi kujiunga na 
Chuo hicho katika maeneo mbalimbali ili waweze kujiendeleza zaidi na 
kuboresha mbinu za ufundishaji.
Alisema
 kuwa Chuo Kikuu Huria kikitumiwa vizuri kinamchango mkubwa wa kuleta 
mageuzi katika sekta ya elimu na nyingine na kuweza kuboresha ufaulu 
hata katika maeneo ambayo wanafunzi walikuwa hawafanyi vizuri katika 
mitihani yao ya kumaliza elimu ya msingi.
Waziri
 Mkuu huyo Mstaafu aliongeza kuwa hatua itasaidia sana kuleta tija 
katika mbinu ufundishaji itakayoasaidia katika kuongeza ufaulu wa 
wanafunzi wote hata wale wenye mahitaji maalumu.
Katika
 hatua nyingine Mkuu huyo wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania amewaagiza 
Wataalamu wake kuangalia jinsi ya kuandaa utaratibu na vigezo vya 
upimaji wa vituo mbalimbali katika matawi yake nchini ili kuona ni Kituo
 gani kimefanya vizuri na Kituo cha mwisho.
Alisema
 kuwa hatua hiyo itawasaidia kujua kama Kituo kimekuwa cha mwisho sababu
 ni nini na kama ni walimu waweze kutatua na hivyo kufanya waweze nao 
kufanya vizuri.
“Kama
 tunavyofanya katika elimu ya msingi na sekondari , nimeagiza Wataalamu 
waangalie jinsi ya kuanza kupima ufaulu wanachuo wetu katika Vituo vya 
Chuo Kikuu Huria ili tujue cha kwanza na cha mwisho…kama kituo kitakuwa 
cha mwisho tujue na sababu, kama ni udhaifu wa wakufunzi tuweze 
kulifanyia kazi” alisema Mkuu huyo wa Chuo.
Naye
 Mkurugenzi wa CKHT Tabora Noel Nkombe alisema kuwa Tawi hilo 
linakabiliwa na tatizo na ukosefu wa majengo kwa ajili ya utoaji wa 
huduma kwa wanachuo , jambo ambalo limewafanya wafanye kazi kwa kuhama 
hama mara kwa mara.
Alisema
 kuwa ili kukabiliana na tatizo hilo tayari wamepata kiwanja katika eneo
 la Ipuli katika Manispaa ya Tabora ambapo katikati ya mwezi ujao 
wanatarajia kuendesha harambee kwa ajili ya kupata fedha za kuanza 
ujenzi wa awali.
Akisoma
 risala ya wanachuo Katibu wa Serikali ya Wanachuo Tawi la Tabora Husna 
Suleyman alisema kuwa kwa kutambua tatizo la majengo kwa ajili ya Kituo 
chao , wao kwa hiari hayo wameamua kuchanga kila mmoja shilingi 30,000 
ambapo zimepatikana milioni 6.1.
Alisema kuwa hatua hii inalenga kuunga mkono juhudi za uongozi wa CKHT za kutaka kuboresha mazingira ya wao kujisomea.
mwisho
Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment