Home » » MWANRI ATOA MWEZI MMOJA KWA WAMILIKI WA KIWANDA CHA MANOGA KUHAKIKISHA KINAANZA KAZI.

MWANRI ATOA MWEZI MMOJA KWA WAMILIKI WA KIWANDA CHA MANOGA KUHAKIKISHA KINAANZA KAZI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Baadhi ya mitambo ya Kiwanda cha Pamba cha Manonga wilayani Igunga ambayo ilikuwa ikutumika kuchambua Pamba na kuzalisha mafuta yake ambayo hafanyi kazi kwa kipindi kirefu baada ya wamiliki wake kusimamisha uzalishaji. Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri( hayupo katika picha) jana ametoa mwezi mmoja mitambo hiyo ianze kufanya kazi.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri (aliye mbele) akiangalia mmoja wa mitambo baaya kutembelea Kiwanda cha Pamba cha Manonga jana wilayani Igunga kwa ajili ya kujionea hali halisi kilivyo hivi na mahitaji yake ili kianze upya uzalishaji.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri (kulia) akibadilishana mawazo na Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Ushirika mkoani Shinyanga (SHIRECU) Robert Mayongela Jongera (kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Igunga John Mwaipopo (kulia) baada viongozi mbalimbali kutembelea Kiwanda cha Pamba cha Manonga jana wilayani Igunga kwa ajili ya kujionea hali halisi kilivyo hivi na mahitaji yake ili kianze upya uzalishaji.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri (kulia) akiwasisitiza wamiliki wa Kiwanda cha Pamba cha Manonga kilichopo wilayani Igunga kuhakikisha ndani ya mwezi mmoja mitambo ya kiwanda hicho iwe imeshaanza kazi. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Igunga John Mwaipopo. Mkuu wa Mkoa alitoa maelezo hayo jana alikwenda kutafuta sababu za kwanini hakiendelei na uzalishaji kwa zaidi ya miaka 20.

Na Tiganya Vincent-RS-Tabora.

SERIKALI ya Mkoa wa Tabora imetoa mwezi mmoja kwa wamiliki wa Kiwanda cha Pamba cha Manonga kuhakikisha wamekikarabati ili kiweze kuanza tena uzalishaji wa mafuta ya pamba na uchambuzi wa Pamba na kutengeneza ajira kwa vijana mkoani hapo.

Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri jana wilayani Igunga wakati alipokwenda kujionea hali halisi ya kiwanda hicho ambacho kwa maika zaidi ya 20 hakifanyi kazi.

Alisema kuwa baada mwezi mmoja huo kukamilika atafanya ziara Kiwandani hapo ili kuhakikisha kama ukarabati umeshakamilika na mitambo imeshaanza kufanya kazi na kinyume cha hapo atalazimika kumwandikia Waziri wenye dhamana na viwanda ili wamiliki wake wanyang’anye kwa ajili ya kumpa mwekezaji mwingine.

Mwanri aliwaagiza Wamiliki wa Kiwanda hicho ambao ni Rajani pamoja na Chama Kikuu cha Ushirika cha Igembensabo kupanga ratiba ya mpango kazi wa utekelezaji shughuli zitakazoonyesha mipango ya ufufuaji na muda wa ukamilishaji kwa ajili kufanikisha zoezi hilo ndani ya muda ulipangwa , vinginevyo watashindwa.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa