Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Baadhi ya mitambo ya Kiwanda cha Pamba cha Manonga wilayani Igunga ambayo ilikuwa ikutumika kuchambua Pamba na kuzalisha mafuta yake ambayo hafanyi kazi kwa kipindi kirefu baada ya wamiliki wake kusimamisha uzalishaji. Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri( hayupo katika picha) jana ametoa mwezi mmoja mitambo hiyo ianze kufanya kazi.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri (aliye mbele) akiangalia mmoja wa mitambo baaya kutembelea Kiwanda cha Pamba cha Manonga jana wilayani Igunga kwa ajili ya kujionea hali halisi kilivyo hivi na mahitaji yake ili kianze upya uzalishaji.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri (kulia) akibadilishana mawazo na Mwenyekiti wa Chama Kikuu cha Ushirika mkoani Shinyanga (SHIRECU) Robert Mayongela Jongera (kushoto) na Mkuu wa Wilaya ya Igunga John Mwaipopo (kulia) baada viongozi mbalimbali kutembelea Kiwanda cha Pamba cha Manonga jana wilayani Igunga kwa ajili ya kujionea hali halisi kilivyo hivi na mahitaji yake ili kianze upya uzalishaji.
Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri (kulia) akiwasisitiza wamiliki wa Kiwanda cha Pamba cha Manonga kilichopo wilayani Igunga kuhakikisha ndani ya mwezi mmoja mitambo ya kiwanda hicho iwe imeshaanza kazi. Kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Igunga John Mwaipopo. Mkuu wa Mkoa alitoa maelezo hayo jana alikwenda kutafuta sababu za kwanini hakiendelei na uzalishaji kwa zaidi ya miaka 20.
Na Tiganya Vincent-RS-Tabora.
SERIKALI
 ya Mkoa wa Tabora imetoa mwezi mmoja  kwa wamiliki wa Kiwanda cha Pamba
 cha Manonga kuhakikisha wamekikarabati ili kiweze kuanza tena 
uzalishaji wa mafuta ya pamba na uchambuzi wa Pamba na kutengeneza ajira
 kwa vijana mkoani hapo.
Agizo
 hilo limetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri jana wilayani 
Igunga wakati alipokwenda kujionea hali halisi ya kiwanda hicho ambacho 
kwa maika zaidi ya 20 hakifanyi  kazi.
Alisema
 kuwa baada mwezi mmoja huo kukamilika atafanya ziara Kiwandani hapo ili
 kuhakikisha kama ukarabati umeshakamilika na mitambo imeshaanza kufanya
 kazi na kinyume cha hapo atalazimika kumwandikia Waziri wenye dhamana 
na viwanda ili wamiliki wake wanyang’anye kwa ajili ya kumpa mwekezaji 
mwingine.
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment