NA TIGANYA VINCENT
RS-TABORA
13 February 2018
SERIKALI
 ya Mkoa wa Tabora imesema mafunzo ambayo yanayotolewa kwa wafugaji wa 
nyuki hapa nchini yamesaidia kuongezeka uzalishaji wa mazao ya asali na 
hivyo kuwepo na uwekezaji katika biashara ya mazao ya nyuki.
Hatua
 hiyo imetokana kuwepo kwa soko kubwa dunia la mazao ya nyuki ambalo 
limefanya kuwepo na chachu kufungua mianya ya wafugaji na 
wafanyabiashara kutaka kujifunza juu ya uzalishaji unaoazingatia ubora 
na unaokubalika kitaifa na kimataifa. 
Kauli
 hiyo jana na Kaimu Katibu Tawala Mkoa wa Tabora Nathilis Linuma wakati 
akifungua mafunzo ya siku tano ya wafanyabiashara wa biadha zinazotokana
 na nyuki katika Chuo cha Nyuki na kuwashirikisha washiriki kutoka 
Mwanza, Simiyu na wenyeji.
Linuma alisema takwimu zinaonesha
 kuwa uzalishaji wa mazao ya nyuki hususani asali na nta unaongezeka 
kutoka tani 9,000 za asali kwa mavuno ya  mwaka 2012  hadi tani 34,000 
za asali kwa mavuno ya mwaka 2016 .
Aliongeza
 kwa mauzo ya nje ya asali yalikuwa tani 103.8 mwaka 2012 na kufikia 
tani 259.9 kwa mwaka 2016 yenye thamani ya Shilingi 2,257,410,880. 
Linuma
 alisema kwa upande wa nta mwaka 2012 iliuzwa tani 277 ambapo hakukuwa 
na ongezeko na kasi kilichouzwa mwaka 2016 ilikuwa ni tani 251.9 yenye 
thamani ya Shilingi 4,549,643,832. 
Kaimu
 Katibu Tawaka huyo wa Mkoa alisema kuwa ongezeko hilo la uzalishaji 
linatokana na mwitikio wa wananchi kupata elimu ya ufugaji wa kisasa na 
kuwekeza katika mashamba ya ufugaji nyuki nchini.
Aidha
 alisema kuwa ili uzalishaji uendelee kuongezeka ni vema wafugaji na 
jamii wakaendelea kuhakikisha wanatunza mazingira na kupanda miti kwa 
wingi ili nyuki wapate chakula cha kuzalishia asali na pia wasaidia 
mimea mashambani.
Kwa upande wa
 Mkuu wa Chuo cha Ufugaji Nyuki Tabora Semu Daud alisema wameamua kutoa 
mafunzo ya muda mfupi kwa wafugaji mbalimbali hapa nchini kwa lengo la 
kuhakikisha kuwa bidhaa wanazozalisha zinakubalika ndani na nje ya 
Tanzania.
Alisema
 wanashirikiana na Shirika la Viwango Tanzania(TBS), Mamlaka ya Chakula 
na Dawa(TFDA) ili kuhakikisha mazao yanayozalishwa yanakuwa yanaviwango 
viwango vinakubalika na Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania 
(TanTrade) kwa ajili ya kuwatafutia masoko ndani na nje ya Tanzania.
Tanzania
 ina maeneo makubwa ambayo ufugaji nyuki unatekelezwa, baadhi ya mikoa 
hiyo ni pamoja na Dodoma, Singida,  Shinyanga, Tabora, Kigoma, Simiyu, 
Mwanza, Katavi na Kagera ambayo inapitiwa na barabara iendayo Burundi, 
Rwanda na Uganda, barabara hii ni fursa kwa mazao ya nyuki kuelekea soko
 la nchi jirani. 
MWISHO 
 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment