Na Tiganya Vincent-rs Tabora
Vitambulisho
 wa uraia vitasaidia kuwa na utambuzi wa wananchi utakao ondoa ile tabia
 ya baadhi ya watu kutilia mashaka wakati wa shughuli mbalimbali ikiwemo
 kipindi kushiriki katika zoezi la uchaguzi wote wote.
Kauli
 hiyo ilitolewa jana mjini Tabora na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, 
Dkt.Mwigulu Nchemba wakati uzinduzi wa zoezi la usajili wananchi kwa 
ajili ya vitambulisho vya kitaifa mkoani humo.
Alisema
 kuwa mara nyingi mtu anapogombea nafasi yoyote hapa nchini au 
kunapokuwepo na migogoro ya kugombania mashamba ndio suala la kusema 
kuwa huyo sio raia linapojitokeza.
Dkt.
 Nchemba alisema wananchi wenye sifa kuchangamkia zoezi la usajili na 
upataji wa vitambulisho vya uraia ili kuepuka matatizo kama vile 
migogoro ikiwemo ya mapingamizi wakati chaguzi mbalimbali na kuiweza 
Serikali kupanga mipango mbalimbali ya maendeleo kwa ajili ya wananchi 
wake
Alisema
 kuwa hata uchumi wa kisasa unaanza na kutambua kwa Serikali kutambua 
watu iliyonao na ndipo ipange mipango ya maendeleo kwa ajili yao.Waziri 
huyo aliongeza kuwa hata kwenye vyombo vya fedha kama vile Benki 
zimekuwa zikiweka riba kubwa katika mikopo kwa sababu ya baadhi wananchi
 kukosa utambulizi
Naye
 Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) 
Andrew Massawe alisema jitihada hizi zote zimelenga kusaidia Serikali na
 wananchi kutambulika na hatimaye Mashirika, Taasisi na Makampuni nchini
 kutumia mfumo huu kutoa huduma zenye ubora na tija kwa Taifa.
Alisema
 mfumo huu una faida nyingi kwa Taifa na mwananchi mmoja mmoja kama vile
 kuimarisha Ulinzi na Usalama wa nchi, wananchi kutambulika kwa haraka 
pindi wanapofika kupata huduma za afya na Elimu.
Massawe
 alisema kuwa faida nyingine ni kurahisisha utambuzi wa makundi yenye 
mahitaji maalumu ikiwemo utambuzi wa kaya masikini unaofanywa na Mfuko 
wa Maendeleo ya Jamii (TASAF) na upatikanaji wa huduma za kifedha na 
Simu kirahisi.
Kwa
 upande wa Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Tabora Queen Mlozi aliwaagiza viongozi 
wa ngazi zote mkoani humo kuhakikisha kuwa anayesajiliwa na kupata 
kitambulisho cha uraia ni yule mwenye sifa na sio mgeni.
Alisema
 Serikali ya Mkoa wa Tabora haitasita kumchukulua mtu yoyote 
atayeshiriki katika udanganyifu utaosababu watu wasio raia kupata 
vitambulisho vya uraia.
Queen
 alisema kuwa kila mmoja ni vema akasimama katika nafasi yake 
kuhakikisha kuwa anafanya kazi kwa umakini na uadilifu wa hali ya juu 
ili kuleta ufanisi.
Alitoa wito kwa jamii kusaidia kuwafichua watu wasio raia wanaotaka kujipenya ili wapate vitambulisho vya uraia
 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment