NA TIGANYA VINCENT
RS TABORA
10 January 2018
WALIMU
 wenye madeni halali mkoani Tabora wametakiwa kuhakikisha wanawasilisha 
vielelezo vinavyoonyesha uhalali wa madai yao kwa Maofisa Elimu waliopo 
karibu nao ili yaweze kufanyiwa kazi mapema.
Kauli
 hiyo ilitolewa jana wilayani Igunga na Katibu Tawala Msaidizi Mkoa wa 
Tabora anayeshughulikia Elimu Suzan Nussu wakati akiongea na walimu wa 
Shule ya Sekondari ya Ziba alipokuwa ameongozana na Mkuu wa Mkoa huo 
 Aggrey Mwanri ili kukagua ujenzi wa mabweni ya wanafunzi.
Alisema
 kuwa ni vema zoezi hilo kilafanyika mapema na kwa makini ili Walimu 
wanaodai madai ya haki waweze kupata fedha zao kama alivyoagiza Rais wa 
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt John Pombe Magufuli hivi 
karibuni.
 “Nawaomba
 walimu wenzangu hakikishe mnawaeleza wenzenu wenye madi kupeleka madai 
yao mapema kwa Maofisa Elimu waliokaribu nao ili nao waweze 
kuyawasilisha mapema Mkoani kwa ajili ya hatua zaidi…ucheleweshaji 
wowote unaweza kuwasababisha walimu wachelewe pia kupata haki yao” 
alisisitiza Nussu.
Aidha
 Katibu Tawala huyo Msaidizi wa Mkoa aliwaonya walimu na Maofisa Elimu 
kutofanya udanganyifu wowote kwani fedha kidogo inaweza ikawasababisha 
wapoteze kazi zao na hata kujikuta katika vyombo vya Sheria.
Alisema
 kuwa walimu wanapopeleka madai yao ni vema wakajiridhisha kuwa ni kweli
 wanadai na madai yao ni kweli ili kujiweka katika mazingira salama.
Nussu
 aliongeza kuwa Maofisa Elimu katika Halmashauri zote za Mkoa wa Tabora 
ni vema wakahakikisha walimu wote wanapata taarifa na wanahusika waweze 
kufikisha taarifa hizo haraka mkoani.
Mwisho
 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment