Home » » RC TABORA ANZENI MAPEMA KUWAANDA WAKULIMA WA PAMBA ILI TUPATE MAVUNO MAZURI.

RC TABORA ANZENI MAPEMA KUWAANDA WAKULIMA WA PAMBA ILI TUPATE MAVUNO MAZURI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri (mwenye shati jeupe ) akiongozana na viongozi mbalimbali kukagua mitambo ya Kiwanda cha Pamba cha Manonga jana wilayani Igunga kwa ajili ya kujionea hali halisi kilivyo hivi na mahitaji yake ili kianze upya uzalishaji.

Na Tiganya Vincent- RS-Tabora

SERIKALI ya Mkoa wa Tabora imeawaagiza Maafisa Ugani kuanza mapema maandalizi ya kilimo cha pamba kwa wakulima kutoka wilaya tano mkoani hapo zilichaguliwa kulima zao ili waweze kuzalisha pamba nyingi na nzuri kwa ajili viwanda mbalimbali hapa nchini.

Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri jana wilayani Igunga wakati alipokwenda kujionea hali halisi ya Kiwanda cha Pamba cha Manonga wilayani Igunga ambacho kimekuwa hakifanyi kazi kwa miaka zaidi ya 20 kwa sababu mbalimbali ikiwemo ukosefu wa pamba ya kutosha.

Alisema kuwa watendaji wote wanaohusika na usimamizi wa zao la pamba ni vema wakahakikisha kuwa wakulima wanapanda mbegu zinazotakiwa na kwa nafasi inayoshauri kitaalamu na kutimia mbolea na dawa za kuua wadudu zinazotakiwa.

Mwanri alisema kuwa Tabora imepata mbegu bora tani 500 ambazo zitasaidia kusambazwa katika Wilaya ambazo zimechaguliwa kulima zao la Pamba za Kaliua, Urambo, Nzega, Igunga na Uyui.

Alisisitiza pamba itakayolimwa na kuvuna itauzwa kupitia Vyama vya Ushirika na sio vinginevyo ili kuepuka mkulima kunyonywa.

Aidha Mkuu huyo wa Mkoa alipiga marufuku matumizi ya mbegu ambazo hazikuidhinishwa na Bodi ya Pamba na kuingiza mkoani hapa dawa ambazo zimepitwa na wakati.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa