Home » » Wanachuo Tumbi wapongezwa kwa kufaulu vizuri

Wanachuo Tumbi wapongezwa kwa kufaulu vizuri

WANACHUO katika chuo cha Kilimo na mifugo Tumbi,Mkoani Tabora wamepongezwa kwa kufanya vizuri katika mitihani ya kumaliza masomo yao chuoni hapo ambapo zaidi ya asilimia 95 wamefaulu.

Akitoa pongezi kwa wanachuo waliomaliza mwaka huu,mwenyekiti wa bodi ya chuo hicho,Bw.Omary Kamulika, amesema kati ya wanachuo 412 waliomaliza mafunzo katika ngazi ya Cheti, wanachuo 401 wamefaulu masomo yao huku kumi na moja wakitakiwa kurudia.

Amesema wanachuo waliomaliza ni lazima wapongezwe kwani pamoja na kukabiliwa na changamoto nyingi lakini wameweza kufanya vema.

Bw,Kamulika amewahakikishia wananchi na wanachuo kwa ujumla kuwa Chuo cha kilimo na mifugo Tumbi kitaendelea kuwa Chuo bora katika kuwaandaa wanachuo ili wawe watumishi wazuri watakaolifaa Taifa.

Kuanzia mwaka huu wa masomo 2013/14 Chuo hicho kitaanza kuchukua wanafunzi wa Diploma wapatao Mia Moja na hamsini huku wale wa ngazi ya cheti wakiwa Mia nne.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa