Home » » Chuo cha ardhi kuanza kutoa wahitimu wanaoendana na mahitaji ya soko la ajira

Chuo cha ardhi kuanza kutoa wahitimu wanaoendana na mahitaji ya soko la ajira

MTAALA mpya wa Masomo wa Chuo cha Ardhi Tabora utawezesha Chuo hicho kutoa wahitimu wenye uwezo wa kufanya kazi bila matatizo tofauti na ilivyo sasa.

Akifunga mafunzo ya Mtaala Mpya wa chuo hicho,Katibu Tawala Msaidizi Mkoa wa Tabora,Bw.Longino Kazimoto,ameagiza Chuo hicho kisajiliwe haraka na NACTE ili mtaala mpya utakapoanza kutumika usaidie kupatikana wahitimu wenye uwezo wa kufanya kazi.

Mkuu wa Taaluma wa Chuo hicho,Bi.Helena Kenekeza,amesema  lengo la mafunzo   ni kukamilisha Mtaala mpya ili wanachuo wanapomaliza wawe mahiri katika kazi zao na wasitegemee mafunzo kazini kama ilivyo sasa.

Kwa upande wao wadau wa mafunzo hayo wamesifu Mtaalama huo Mpya utakaoanza kutumika kuwa utakifanya Chuo kuwa na sifa nzuri kwani kitakuwa na uwezo wa kutoa wahitimu wenye ubora wanaojua kufanya kazi.

Chuo cha Ardhi Tabora kinatoa mafunzo katika ngazi ya Cheti na Stashahada katika fani mbalimbali za Ardhi,kikikabiliwa na changamoto ya ukosefu wa uzio,Nyumba za watumishi,Gari na zahanati kwa ajili ya kuwahudumia wanachuo na watumishi.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa