Home » » ‘Wasipowalipia CHF wanyimeni unyumba’

‘Wasipowalipia CHF wanyimeni unyumba’

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
MKUU wa Wilaya ya Igunga, Elibariki Kingu, amewataka wanawake walioolewa wilayani humo kuwagomea waume zao endapo watakataa kulipa fedha za kujiunga na Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF).
Alisema mafanikio ya mgomo wa kina mama kwa wanaume wanaokataa kuziunganisha familia zao na huduma ya CHF utawafanya wajiunge na huduma hiyo ili kuwapa uhakika wa matibabu ya dharura pindi wanapokosa fedha.
“Tunawahimiza wote kina baba na kina mama mjiunge na huduma hii na kina mama ninyi na watoto wenu ndio waathirika wakubwa wa kukosa fedha za matibabu kwa wakati.

Chanzo;Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa