Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 MKUU wa Wilaya ya Igunga, Elibariki Kingu, amewataka wanawake 
walioolewa  wilayani humo kuwagomea waume zao endapo watakataa kulipa 
fedha za kujiunga na  Mfuko wa Afya ya Jamii (CHF).
  Alisema mafanikio ya mgomo wa kina mama kwa wanaume wanaokataa 
kuziunganisha  familia zao na huduma ya CHF utawafanya wajiunge na 
huduma hiyo ili kuwapa  uhakika wa matibabu ya dharura pindi wanapokosa 
fedha.
  “Tunawahimiza wote kina baba na kina mama mjiunge na huduma hii na 
kina mama  ninyi na watoto wenu ndio waathirika wakubwa wa kukosa fedha 
za matibabu  kwa wakati.
Chanzo;Tanzania Daima  
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment