Home » » Agizo la Rais Dkt. Magufuli latekelezwa kwa vitendo Igunga

Agizo la Rais Dkt. Magufuli latekelezwa kwa vitendo Igunga


Na Godfriend Mbuya
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli wakati wa ziara yake mkoani Tabora alitoa maagizo kadhaa kwa watendaji likiwemo agizo la kufunguliwa kwa stendi ya mabasi Igunga ambayo ilikamilika na kuacha kutumiwa kwa miaka 10.
Kufuatia agizo hilo tayari SUMATRA kwa kushirikiana na jeshi la polisi kikosi cha usalama barabarani wameanza kuelekeza magari yote ya abiria uyanayopita Tabora eneo la stendi hiyo kuhakikisha yanapita jambo ambalo limeanza kufanyiwa kazi kwa vitendo.
Akizungumza wakati wa kukagua utekelezaji wa agizo hilo Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri amesema SUMATRA washirikiane na jeshi la polisi kuhakikisha kila gari la abiria linapita na dereva atakayekaidi agizo hilo anyang'anywe leseni.
Ni lazima mabasi yapite hapa stendi na yeyote atakayekaidi SUMATRA chukueni hatua na jeshi la polisi toenio ushirikiano kuhakikisha suala hili linafanikiwa'' Amesema Mwanri.
Aidha kwa upande wao wananchi wamesema watanufaika sana kufuatia stendi hiyo kuanza kufanya kazi kwa kuwa watafanya biashara mbalimbali kuzunguka stendi hiyo.
You might also like:

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa