Home » » WAJASIRIAMALI NZEGA WAPEWA MIL.20 / -

WAJASIRIAMALI NZEGA WAPEWA MIL.20 / -

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.

Imeandikwa na Basil
KAMPUNI ya simu za mkononi ya Airtel kupitia mfuko wake maalumu wa kusaidia jamii wa Airtel FURSA Tunakuwezesha, imekabidhi hundi ya Sh milioni 20 kwa Mbunge wa Nzega Mjini, Hussen Bashe, kuwanufaisha wajasiriamali jimboni humo.
Akikabidhi hundi hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa Airtel, Sunil Colasa alisema, “Airtel imejipanga kuhakikisha vijana wanaendelea kunufaika na mradi wa Airtel FURSA kwa kuwapatia misaada ya kukamilisha mipango yao waliyoipanga ya kupunguza changamoto walizonazo ikiwamo ya ukosefu wa ajira na mtaji ili watimize malengo yao kibiashara”.
Bashe aliishukuru Airtel na kuahidi kusimamia mradi huo wa ukopeshaji kwa ajili ya kuweza kuinua vipato vya wananchi wa Nzega kama ilivyokusudiwa.
Mradi wa Airtel Fursa, ulianzishwa Mei mwaka jana na tayari umewafikia vijana zaidi ya 5,000 kutoka katika mikoa 10 nchini pamoja na vijana 100 waliowezeshwa kwa kupewa mitaji na vitendea kazi.
Programu hii kati ya Airtel na Mfuko wa Maendeleo Nzega chini ya Mbunge wa Jimbo la Nzega Mjini, Bashe, itawawezesha zaidi ya wajasiriamali 350 kunufaika na mikopo kupitia huduma ya Airtel Money.
CHANZO :HABARI LEO

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa