Home » » RC TABORA: MA-DED NUNUENI VIFAA VYA KUPIMIA UBORA WA UDONGO ILI KUWASAIDIA WAKULIMA

RC TABORA: MA-DED NUNUENI VIFAA VYA KUPIMIA UBORA WA UDONGO ILI KUWASAIDIA WAKULIMA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.


Na  Tiganya Vincent – TABORA

SERIKALI ya Mkoa wa Tabora imewaagiza Wakurugenzi Watendaji wa Manispaa na Halmashauri kuhakikisha wanawanulia Maafisa Ugani vifaa vya kupimia ubora wa udongo(soil kits ) kwa ajili ya kuwawezesha kutoa huduma ya ushauri kwa wakulima ili waendeshe kilimo kulingana na hali ya udongo wa eneo husika.

Kauli hiyo ilitolewa jana mjini hapa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri wakati akifunga mafunzo ya siku saba ya Maafisa Ugani kutoka Halmashauri zinazolima zao la tumbaku kwa lengo la kuwajengea uwezo wa kutoa huduma nzuri kwa wakulima. Alisema kuwa vifaa hivyo ni lazima vinunuliwe walau vichache vya kuanzia ili Maafisa Ugani katika ngazi za kuanzia kijiji hadi Kata waweze kuwasaidia wakulima juu ya matumizi sahihi ya pembejeo ikiwemo mbolea katika udongo husika kwa ajili kuwafanya wazalishe mazao mengi.

Mwanri aliongeza kuwa wakulima wamekuwa hapati mafanikio wakati mwingine kwa sababu ya kukosa wataalamu wa kuwashauri jinsi ya kuendesha kilimo cha kulingana na udongo walionao katika eneo lao na matumizi sahihi ya pembejeo kulingana na hali halisi ya udongo.

“Vifaa hivyo vitasaidia wao kujua ni virutubisho gani vinapungua katika udongo na hivyo waweze kumshauri mkulima jinsi ya kuongeza virutubisho hivyo ili apate mafanikio na kuachana na kilimo cha kukisia katika matumizi ya pembejeo”alisisitiza Mkuu wa Mkoa huyo.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa