Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Na Tiganya Vincent
WATU
 saba wa kijiji cha Mwambondo wilayani Uyui wanashirikiliwa na Jeshi la 
Polisi kwa tuhuma za kuwashambulia na kuwauunguza kwa moto wanawake 
waanne wakiwatuhumu kuwa wachawi na wanahusika na kifo cha mume wa mmoja
 wao.
Kauli
 hiyo imetolewa jana mjini hapa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri 
wakati wa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu taarifa alizozipata 
kutoka kwa Kamanda wa Polisi Mkoa huo Wilbroad Mtafungwa.
Alisema
 kuwa chanzo cha vitendo hivyo vya kinyama zilianzia baada ya Mtu mmoja 
alikuwa akiitwa Mafumba Jirawisi kufariki  kwa sababu ya maradhi lakini 
baadhi ya watu walianza kumtuhumu mke wa marehemu anayeitwa Manugwa 
Lutema kuhusika na kifo cha mume wake na kuamua kumpeleka porini na 
kuanza kumshambulia huku wakitaka awaeleze watu wanaoshirikiana naye 
kuwafanya vitendo vya kichawi.
Mwanri
 alisema kuwa mama huyo baada ya kupiga sana na kuumia aliamua kutaja 
ovyo majina ya majirani zake na ndipo nao wakaunganishwa naye na 
kuendelea kupigwa na kuunguzwa katika sehemu za siri.
Kufuatia
 vitendo hivyo vya kinyama Mkuu huyo wa Mkoa amemwagiza kuwasaka watu 
waliobaki ambao wamehusika katika kitendo hicho wakiwemo Makamanda wa 
sungusungu ili hatua kali ziweze kuchukuliwa dhidi yao.
Mmoja
 wa majeruhi wa tukio hilo la kinyama alisema kuwa alilazimika kutaja 
majirani zake ili kutaka kunusu roho yake baada ya kuona mashambulizi 
yanazidi na anasikia maumivu makali.
Kwa
 upande wa ndugu wa waathiri wameomba wagonjwa wao watibiwe bure kwa 
sababu tukio hilo limetokea wakati wakiwa hawana kitu na hawajiandaa na 
kutokuwa na fedha ya kulipia matibabu
Akijibu
 ombi la ndugu hao Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tabora Dkt. Gunin Kamba 
alisema wagonjwa wote walijeruhiwa na kuuguzwa moto watapewa matibabu 
kwa mkopo katika Hospitali hiyo ya Rufaa ya Mkoa ya Kitete ,malipo 
yatafanyika baadaye.
Alisema kuwa lengo ni kutaka kwanza kuokoa maisha yao kutokana na unyama waliofanyiwa na kundi hilo la watu.
Naye
 Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Kitete Dkt.Nassor Kaponta alisema kuwa 
wanaendelea kuwapatia huduma katika Hospitali hiyo na hakuna majeruhi 
ambaye atahamishiwa kwingine kwa sababu wanauwezo wa kuwasaidia wakiwa 
katika eneo hilo hilo.
Aliwataja waliojeruhiwa ni Maria Sahani , Elizabeth Kashindye, Manugwa Lutema na Raheli Mikomangwa. Kabla
 ya kufariki marehemu ambaye alikuwa mganga wa kienyeji alikwenda kutoa 
matibabu kijiji cha jirani na baada ya kurejesha akaanza kuumwa na 
hatimaye usiku wake alifariki kwa sababu ya ugonjwa.
Vitendo
 vya kinyama ikiwemo mauaji kwa wanawake Mkoani Tabora vinaanza 
kuonekana kama vya kawaida ambapo mapema mwezi Agosti mwaka huu wilayani
 Nzega wakinamama watano walipoteza maisha baada ya kushambuliwa na 
kisha kuchomwa moto na mwei huo huo wilayani Sikonge mtu mmoja 
alinusurika kifo baada ya kufungiwa nyumbani kwake na nyuma kuwekwa moto
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment