Na Tiganya Vincent
RS-Tabora
9 Novemba 2017
SERIKALI
 ya Mkoa wa Tabora imesema itakamata mali za  Kampuni zilizopewa jukumu 
la kusambaza pembejeo kwa ajili ya wakulima wa pamba ambao 
watawasambashia hasara wakulima ambao watawasambazia mbegu mbovu za 
pamba ambazo hazitaota na dawa ilisoua wadudu.
Kauli
 hiyo imetolewa hivi karibuni na Mkuu wa Mkoa wa Tabora wakati wa ziara 
yake ya kuwaelimisha wakulima wa pamba katika Wilaya ya Uyui.
Alisema
 kuwa hawezi kukubali wakulima wapate hasara na yeye akiwa kiongozi 
anayebeba dhamana ya kuhakikisha kuwa anatumia vyombo vyote 
vinavyomsaidia na kumshauri katika kulinda maslahi ya umma wakiwemo 
wakulima wa pamba.
 “Kampuni
 itakayo sambaza mbegu ambazo hazioti na dawa ambazo haziui wadudu 
nitamkamata yeye na  mali zake zote ikiwemo magari na kupiga mahesabu ya
 hasara waliyopata wakulima na kisha nitamwaandikia invoice   ili aweze 
kulipa gharama ya hasara hiyo ndio nitamwachia yeye na mali zao” alisema
 Mwanri.
Alisema
 kuwa hesabu hiyo itahusu kulipa fedha ambazo mkulima angepata kutokana 
na kilo ambazo angezalisha katika eneo lake na kwa kuzingatia bei ya 
ununuzi wa pamba wa wakati wa mauzo.
Kwa
 upande wa Meneja Mbegu kutoka Kampuni ya Usambazaji Mbegu ya Quoton 
Tanzania Limited Phineas Chikaura alimwahakikishia Mkuu huyo wa Mkoa 
kuwa aina ya mbegu ni salama na kuwaomba wakulima kutochimba mashimo 
marefu wakati wa upandaji wa mbegu za pamba kwa sababu zao hilo halina 
nguvu za kusukuma udongo kama yalivyo mazao mengine.
Alisema kuwa wakichimba mashimo marefu upo uwezekano wa mbegu kushindwa kuotoa na kudai kuwa ni mbovu.
Chikaura
 aliongeza kuwa pia wakulima hawapaswi kuloweka mbegu za pamba kabla ya 
kupanda bali wanapaswa kugonja mvua inyeshe ndio wapande.
Alisema
 kuwa kitendo cha kuloweka wakati mwingine usababisha mbegu ishindwe 
kuotoa endapo mvua ikichelewa kunyesha katika eneo husika,
 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment