Wanafunzi
 wa Shule ya Msingi ya Shila Wilayani Nzega mkoani Tabora wakiwa 
wamebeba mbegu ya Viazi lishe wakielekea kwenye shamba darasa wakati wa 
uzinduzi wa shamba hilo wilayani humo leo. Shule hiyo ni shule pekee 
wilayani humo kupata bahati ya kuanzisha shamba hilo.
 Mwakilishi
 wa Kaimu Mkurugenzi wa COSTECH ambaye ni Ofisa Mwandamizi wa COSTECH, 
Audax Mutagwa (kulia), akimkabidhi mbegu ya mihogo Mkuu wa Wilaya ya 
Nzega, Godfrey Ngapula kwa ajili ya kupandwa katika mashamba darasa 
katika uzinduzi wa mashamba hayo ya mbegu wilayani humo leo. 
 Wanafunzi wa Shule ya Shila wakiwa shambani wakati wa uzinduzi wa shamaba darasa hilo.
 Ofisa
 Kilimo kutoka Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Said Babu akizungumza 
kabla ya kuanza uzinduzi huo uliofanyika katika Wilaya hiyo Shule ya 
Msingi, Shila.
 Mwakilishi wa Kaimu Mkurugenzi wa COSTECH ambaye ni Ofisa Mwandamizi wa COSTECH, Audax Mutagwa, akizungumza katika uzinduzi huo.
 Mtafiti
 wa mazao ya mizizi kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Maruku mkoani
 Kagera, Jojianas Kibura, akielezea ubora wa mbegu ya mihogo 
iliyofanyiwa utafiti kabla ya uzinduzi wa shamba darasa katika Shule ya 
Msingi ya Shila.
 Kaimu Ofisa Ugani wa Halmshauri ya Wilaya ya Nzega, Hassan Mtomekela akizungumza katika uzinduzi huo.
 Mtafiti
 wa mazao ya mizizi kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Maruku mkoani
 Kagera, Jojianas Kibura, akielekeza jinsi ya kupanda mbegu ya mihogo 
hiyo kiutaalamu.
 Mtafiti
 wa mazao ya mizizi kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Maruku mkoani
 Kagera, Jojianas Kibura, akimuonesha mbegu hiyo mkuu wa wilaya hiyo.
 Mkuu wa Wilaya hiyo akizindua shamba darasa hilo kwa kupanda mbegu ya mihogo katika Shule ya Msingi ya Shila.
 Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, Gunguti Awadh Mzee akipanda mbegu hiyo.
 Dada Mkuu wa Shule ya Shilwa, Maria Kulwa akipanda mbegu hiyo.
 Upandaji ukiendelea katika shamba hilo.
 Mwalimu
 Mkuu wa Shule hiyo, Gunguti Awadh Mzee, akizungumza na waandishi wa 
habari kuhusu bahati iliyopata shule yake kwa kupatiwa mradi huo wa 
shamba la mbegu.
 Mkulima wa Kijiji cha Shila, Zainabu Kanijo akizungumza na wanahabari.
 Wanawake
 wa Kikundi cha Wasafi Camp Imala Makoye kilichopo Kijiji cha Iyombo 
Kata ya Utwigu wakiwa wamebeba mbegu ya Viazi lishe wakielekea kupanda 
katika shamba darasa.
 Mtafiti
 wa mazao ya mizizi kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Maruku mkoani
 Kagera, Jojianas Kibura, akiwaelekeza wanakikundi hicho jinsi ya 
kupanda mbegu hiyo.
 Wanawake
 wa Kikundi cha Wasafi Camp Imala Makoye kilichopo Kijiji cha Iyombo 
Kata ya Utwigu wakipanda mbegu hiyokatika shamba lao.
 Wanawake
 wa Kikundi cha Wasafi Camp Imala Makoye kilichopo Kijiji cha Iyombo 
Kata ya Utwigu wakiimba nyimbo za kabila la kisukuma kufurahi mbegu 
hiyo.
Mtafiti
 wa mazao ya mizizi kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Maruku mkoani
 Kagera, Jojianas Kibura, akiwaelekeza wakulima wa Kijiji cha Upungu 
Kata ya Puge jinsi ya kupanda mbegu ya mihogo
Na Dotto Mwaibale, Nzega Tabora
MKUU wa Wilaya ya Nzega mkoani Tabora, Godfrey Ngapula amesema Sayansi na Teknolojia haiwezi kuepukika katika kilimo nchini.
Ngapula
 ameyasema hayo leo kwenye uzinduzi na kukabidhi mbegu bora za Mahindi 
ya Wema 2109, mihogo na Viazi lishe kwa ajili ya kuanzisha mashamba 
darasa katika vijiji vya Shila, Iyombo, Upungu, Lububu na Kapanga 
wilayani humo.
Mkuu
 huyo wa wilaya alisema ili kufanya kilimo chenye tija sayansi na 
teknolojia haiwezi kuepukika kutokana na changamoto mbalimbali zilizopo.
Alisema
 kilimo cha kisayansi kina tija kwani mkulima anaweza kulima eneo dogo 
na kupata mavuno mengi kuliko kilimo cha mazoea ambacho mkulima hulima 
shamba kubwa mazo kidogo.
Ngapula
 aliipongeza Tume ya Taifa ya Sayansi na Teknolojia (COSTECH) kwa 
kuwapelekea mbegu hizo kwa kushirikiana na Jukwaa la Bioteknolojia kwa 
Maendeleo ya Kilimo (OFAB) 
Akizungumzia
 matumizi ya mbegu zilizozalishwa kwa teknolojia  ya uhandisi jeni (GMO)
 alisema hayakwepeki kwa kuwa mbegu hizo zinasifa ya kukabiliana na 
changamoto mbalimbali ikiwemo ukame na wadudu waharibifu wa mazao.
Alisema
 wilaya hiyo kupelekewa mbegu hizo kwao ni fursa kubwa na kwa 
kushirikiana na wakulima na maofisa ugani atahakikisha mashamba darasa 
hayo yanatunzwa vizuri na kuwa ndio chanzo za kutoa mbegu nyingi na 
kuzisambaza katika maeneo mengine.
Mtafiti
 wa mazao ya mizizi kutoka Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha Maruku mkoani
 Kagera, Jojianas Kibura aliwaambia wakulima hao kuwa hekta moja ya 
mihogo iwapo watalipa kwa kufuata ushauri wa wataalamu wataweza kupata 
tani 25 hadi 32 kwa zao la mihogo na viazi lishe watapata tani 7 hadi 9 
kwa hekta moja.
Alisema
 matokeo hayo watayapata endapo watafuata kanuni bora za kilimo cha 
mazao hayo kwa kuzingatia nafasi kati ya mche na mche na mstari kwa 
mstari na matumizi ya mbolea hivyo wataweza kuongeza uzalishaji zaidi 
tofauti na sasa ambapo kwenye hekta moja ya mihogo wanapata tani nane 
hadi kumi wakati kwenye viazi lishe wanapata tani moja hadi 3.
Mtafiti
 huyo alisisitiza kuwa mbegu hiyo ya Mihogo ya Mkombozi imefanyiwa 
utafiti na kuonekana kustahimili magonjwa hatari ya mihogo ya batobato 
kali na michirizi ya kahawia ambayo imekuwa ikiwapatia hasara kubwa 
wakulima wengi na kupoteza hadi asilimia 90 za mazao.
Akizungumzia
 kuhusu mbegu Mwakilishi wa Kaimu Mkurugenzi wa COSTECH ambaye ni Ofisa 
Mwandamizi wa COSTECH, Audax Mutagwa, alisema mbegu hizo ya mihogo aina 
ya Mkombozi imefanyiwa utafiti na kuonekana ina uwezo mkubwa wa 
kustahimili magonjwa kama ya batobato kali na michirizi ya kahawia 
ambayo imekuwa ikiwapatia hasara kubwa wakulima na ya mahindi 
ikistahimili hali ya ukame na kutoa mazao mengi.
Mutagwa
 aliwaomba wakulima hao kuyatunza mashamba hayo ambayo yamegharimu fedha
 nyingi hadi kukamilika kwake hivyo wayaendeleze kwa ajili ya kuja kutoa
 matunda kwa wakulima wa wilaya hiyo na kupata chakula cha kutosha na 
ziada kuuza.
Aliongeza
 kuwa kazi kubwa ya COSTECH ni kuishauri serikali katika masuala 
mbalimbali ya sayansi na teknolojia na kuhakikisha matokeo ya tafiti 
zinazofanyika nchini yanawafikia walengwa ambao ni wakulima.
Mwalimu
 Mkuu wa Shule ya Msingi ya Shila ambayo ni shule pekee iliyopata baada 
ya kuwa na shamba darasa la mihogo katika wilaya hiyo,  Gunguti Awadh 
Mzee alisema shamba hilo litakuwa la mfano na kuwa mradi huo utasaidia 
kuwapatia wanafunzi wake chakula wakiwa shuleni hapo.
 
 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment