NA TIGANYA VINCENT
RS TABORA
21 November 2017.
MWANACHUO mmoja Chuo cha Utumishi wa Umma –Tawi la Tabora kinachojulikana kama Uhazili  Raphael Kadesha (22)  amefariki dunia baada ya kujinyonga kwa kutumia tai ya kuvaa shingoni.
Kwa
 mujibu wa Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora Graifton Mushi tukio 
hilo limetokea leo saa 4 asubuhi ambapo marehemu alifunga tai juu ya 
kitanda chake.
Alisema kuwa marehemu alikuwa akisoma kozi cha Cheti cha Awali cha Utawala katika Chuo hicho.
Mushi
 aliongeza kuwa chanzo cha kifo hicho hakijulikani na Jeshi la Polisi 
linaendelea na uchunguzi kujua nini kilimfanya mwanachuo huyo kuchukua 
maamuzi hayo yaliyoacha simanzi katika jamii yake na Chuo kwa ujumla.
Alitoa
 wito kwa wanachuoni kuomba ushauri kwa viongozi wao Chuo au wa kiroho 
pindi wanapokuwa na matatizo binafisi kwani kujiua sio suluhisho la 
matatizo bali ni kuwaongezea walezi wao shida na majonzi zaidi.
Mushi alisema kuwa mwili wa marehemu umehifahiwa katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Kitete.
Naye Mkurugenzi wa  Chuo
 hicho Dkt. Ramadhani Marijani alitoa wito kwa wanachuo kuwa watulivu 
wakati Jeshi la Polisi likiendelea na uchunguzi wa sababu zilizopelekea 
mwanachuo huyo kuchukua maamuzi yaliyoacha simamazi sio tu kwa familia 
yake bali hata kwa Jumuiya nzima ya Uhazili.
Alisema
 kuwa ni vema kama kuna mwanachuo yoyote anakuwa na tatizo au msongo wa 
mawazo kuwaeleza viongozi wake wawe wa Serikali ya Wanafunzi, Mama 
Mlenzi, Mshauri wa Wanachuo au Mkurugenzi mwenye ili waweze kusaidia 
katika ushauri utakaowapa ufumbuzi kuliko kuchukua maamuzi ya haraka.
 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment