NA TIGANYA VINCENT
RS –TABORA
21 NOVEMBA 2017
SERIKALI ya Mkoa wa Tabora izimetaka Halmashauri zote kuanza mara moja utekelezaji wa agizo la ujenzi  na uibuaji wa viwanda visivyopungua 12 katika kipindi mwaka mmoja kuanzia mwezi ujao katika maeneo yao.
Agizo
 hilo limetolewa jana na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey Mwanri wakati 
akizungumza na Viongozi na Watendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga.
Alisema
 kuwa ni vema kila Mkurugenzi Mtendaji anapaswa kukahikisha kuwa anaanza
 mara moja utekelezaji wa agizo hilo la ujenzi wa viwanda ili ifikapo 
mwishoni mwa mwaka ujao kila eneo liwe na viwanda vipya.
Mwanri alisisitiza kuwa wanatakiwa kuhakikisha kuwepo na viwanda vipya vidogo na vya kati kulingana na maagizo ya viongozi.
Alisema
 kuwa hatua itawezesha kusaidia vijana wengi kupata ajira au kujiari 
katika viwanda hivyo vitakavyoanzisha na kuwezesha kufikia nchi ya 
uchumi wa kati kupitia ujenzi wa viwanda.
Mwanri
 alisema katika kufanikisha dhana ya ujenzi wa uchumi wa viwanda, 
Maafsia Ugani wote katika kipindi hiki cha msimu wa mvua watakiwa kwenda
 vijijini kuwasaidia wakulima ili wawaze kuzalisha malighafi nyingi za 
kilimo.
Alisema
 kuwa Mkoa wa Tabora unaendelea kusisitiza kilimo cha mazao kama vile 
alizeti, mihogo, mpunga, korosho, maembe, karanga kwa ajili ya 
upatikanaji wa malighafi za viwandani. 
Kwa upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Kaliua Revocatus Kuuli alisema tayari wataalamu wake wameshaanza kubainisha viwanda vipya ambavyo wataanzisha katika eneo hilo.
Kwa upande wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya Kaliua Revocatus Kuuli alisema tayari wataalamu wake wameshaanza kubainisha viwanda vipya ambavyo wataanzisha katika eneo hilo.
Alisema kuwa kwa upande wao wanatarajia kuvuka lengo na kuwa na viwanda vingi ambavyo vitasaidia kutoa ajira kwa vijana wa eneo.
 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment