Na Tiganya Vincent
RS-Tabora
21 Novemba 2017
WAKURUGENZI
 Watendaji wameagiza kuhakikisha maeneo ya Shule na Taasisi nyingine za 
elimu yanapimwa haraka na kuwekewa mipaka ili kuepuka uvamimizi 
unaofanywa na watu na kusababisha migogoro ambayo imekuwa ikichelewesha 
maendeleo.
Kauli hiyo imetolewa hivi karibuni mkoani Tabora na Naibu
 Katibu Mkuu (ELIMU) Ofisi ya Rais , Serikali za Mitaa na Tawala za 
Mikoa( TAMISEMI ) Tixon Nzunda wakati akizungumza na Watendaji  na watumishi wa Mkoa huo.
Alisema kuwa hatua hiyo itasaidia kuondoa migogoro kati ya uongozi wa Shule husika na wavamizi wa maeneo hayo.
Nzunda
 alisema kuwa migogoro inayotokana na uvamizi wa maeneo ya shule imekuwa
 ikiathiri maendeleo ya wanafunzi na taaluma kwa sababu uongozi wa shule
 wakati mwingine umekuwa ukishindwa kupanua miundo mbinu kwa ajili ya 
utoaji wa elimu kwa wanafunzi.
Alisema
 kuwa ili kuepuka tatizo hilo kuendelea kujitokeza katika maeneo 
mbalimbali ya shule ni kwa Wakurugenzi Watendaji kwa kushirikiana na 
watendaji wengine kama vile watu wa mipango miji kuhakiki maeneo yote 
yanamilikiwa na Shule na kuwaondoa ambao wameingia.
Aidha
 Naibu Katibu Mkuu huyo aliwaagiza Wakuu wote wa Shule kuhakikisha kuwa 
maeneo yao yanapandwa miti mipakani na maeneo mengine ya shule ikiwa ni 
hatua ya kukabiliana na uvamizi unaofanywa na watu wanaoingia baada ya 
kuona maeneo hajafanyiwa uendeleza wowote.
Aliongeza
 kuwa pia wanatakiwa kupanda maeneo ya shule maua ikiwa ni sehemu ya 
kufanya mazingira yavutie wanafunzi kwenda kujifunza.
Katika hatua nyingine Naibu Katibu Mkuu huyo amewaagiza walimu kuhimiza pia masomo ya michezo na Sanaa  mashuleni ikiwa ni sehemu ya kuwavutia wanafunzi wengi kuhudhuria shuleni.
Alisema
 kuwa ni vema wakatumia fedha kidogo wanayopata kununulia vifaa vya 
michezo na Sanaa ili kuwapa fursa wanafunzi kuonyesha vipaji vyao mapema
 ambavyo vinaweza kuwasaidia katika maisha yao ya baadaye kama 
vitaandaliwa na kulelewa vizuri toka awali.
Nzunda alisisitiza kuwa michezo na Sanaa ni sekta  ambazo
 zimesaidia vijana kujiari sehemu mbalimbali duniani , hivyo ni vema 
walimu wasaidie kuwaandaa wanafunzi ili waweze kushiriki kikamilifu 
katika eneo hilo.
Naye
 Mkurugenzi Mtendaji wa Manispaa ya Tabora Bosco Nduguru alisema kuwa 
kwa upande wao wameshaanza kuwaondoa wavamizi wa maeneo ya Shule ambapo 
hivi karibuni waliowaondoa wavamizi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana 
ya Tabora kwa kuvunja nyumba zilizojengwa katika eneo hilo.
Alisema
 kuwa wanataraji kuwaondoa wakati wowote waliovamia maeneo mengine ya 
Shule kama wale wa Shule ya Sekondari MIlambo na kwingineko na kisha 
kuweka uzio.
 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment