NA TIGANYA VINCENT
RS-TABORA
21 November 2017
SERIKALI
 imepiga marufuku Halmashauri zote nchini kuingia makubaliano na 
Mashirika yasiyokuwa ya kiserikali(NGO’S) bila kupitia na kiuhidhinishwa
 na Ofisi ya Rais , Serikali za Mitaa na Tawala za Mikoa( TAMISEMI ) kwa kuwa baadhi ya mambo yamekuwa hayazingatia  vipaumbule vya Serikali  na kuokuwa na manufaa kwa jamii.
Kauli hiyo imetolewa hivi karibuni mkoani Tabora na Naibu
 Katibu Mkuu (ELIMU) Ofisi ya Rais , Serikali za Mitaa na Tawala za 
Mikoa( TAMISEMI ) Tixon Nzunda wakati akizungumza na Watendaji  na watumishi wa Mkoa huo.
Alisema kuwa  mashirika
 hayapaswi kuanza kazi katika Halmashauri yoyote kabla ya mpango kazi 
wao hajaonwa na viongozi wa TAMISEMI ili kujidhirisha kama kweli malengo
 yao yanaendana na vipaumbele vya Serikali vya kuboresha maisha ya 
watanzana Watanzania ambao maisha yao yako chini. 
Nzunda alisema baadhi ya mashirika hayo yamekuwa yakidai kusaidia Watanzania ,lakini matokeo yake  ni kuwanufaisha viongozi wa mashirika hayo na wachache. 
“Kwa
 mfano Mashirika hayo yanapokuja kutaka fulani kama vile elimu ni vema 
yakajua kuwa vipaumbele vya Serikali …….mfano kuboresha miundo mbinu ya 
kujifunzia na kufundishia, kuwajengea uwezo walimu, kuwepo na vifaa vya 
kufundishia na kuweka mazingira mazuri kwa watoto wenye mahitaji 
kujifunza na kusoma katika mazingira rafiki” alisema Nzunda
Alisema
 kuwa wanapoaandika taarifa kwenda kwa watu waliowawezesha fedha 
wanaonyesha kuwa wamewasaidia Watanzania katika miradi ya maendeleo ya 
mabilioni ya fedha kumbe sio kweli fedha nyingi zimeshia mifukoni kwa 
wachache na unapoenda katika eneo ambalo wanadai kusaidia hakuna kitu.
Nzunda
 alisema kuwa Serikali inelenga kuhakikisha kuwa kama fedha zinatolewa 
kwa ajili ya walemgwa ziende kusaidia eneo husika na kama wafadhili 
wanapokuja waone kuwa fedha waliotoa imefanya kazi inayoonekana na sio 
maelezo yasiyo na ushahidi.
Alisema
 kuwa Serikali inapenda kushirikiana na wadau mbalimbali lakini ni vema 
wadau hao watambue kuwa vipo vipaumbele ambavyo inavikusudia katika 
kuwaletea maendeleo watu wake.
Katika
 hatua nyingine Naibu Katibu Mkuu huyo ameagiza kuwa majengo yote 
yanayojengwa katika Shule na Taasisi mbalimbali za elimu yawe rafiki kwa
 watu wenye mahitaji maalumu na watoto wa kike ili kuondoa vikwazo vya 
wao kupata elimu.
Alisema
 kuwa baadhi ya majengo yamekuwa yakisababu wanafunzi wenye mahitaji 
maalumu kushindwa kuhudhiria masomo yao vizuri na kukwamisha ndoto zao 
za kuapata elimu.
Nzunda
 alisema kuwa yapo majengo ambayo yamekuwa hayana maeneo mazuri kwa 
ajili ya watoto wa kike na kuwafanya washindwe kuhudhuria masomo katika 
kipindi Fulani cha mwezi.
 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment