na Moses Mabula, Tabora
WATAALAMU wa
maabara za tiba Tanzania (MeLSAT), wametakiwa kutojiingiza katika siasa na
badala yake wajikite zaidi katika kazi yao ya kutoa huduma kwa wagonjwa.
Wito huo
ulitolewa jana na Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Fatuma Mwassa, alipokuwa akifungua
kongamano la 26 la sayansi na mkutano mkuu wa mwaka wa MeLSAT uliofanyika
katika ukumbi wa Chuo cha Utumishi wa Umma mjini Tabora.
Alisema
mtaalamu wa maabara kujihusisha na siasa ni kutoitendea haki jamii, hivyo
akawataka kuacha mara moja tabia hiyo, ili kuongeza ufanisi kazini.
“Huwa inauma
sana wanasayansi kujiingiza katika masuala ya siasa, na nilikuwa nasubiri
mahala pa kusemea, sasa leo nimepata sehemu hii napenda sana nisisitize jambo
hili, achani kabisa kutamani siasa, mtaua watu ninyi ni watu muhimu sana kwa
taifa,” alisisitiza Mwassa.
Alitaka
kongamano hilo liwe chachu ya kuleta mabadiliko katika sekta ya maabara za tiba
hapa nchini na kwamba wataweza kupata fursa ya kubadilishana uzoefu, kuwajengea
uwezo zaidi wa kuwahudumia wagonjwa pamoja na kujadili changamoto
zinazowakabili sehemu zao za kazi.
Awali, Rais wa
chama hicho, Sabas Mrina, alisema kongamano hilo limelenga zaidi kuimarisha
ushirikiano ili kuendelea kutoa huduma bora zaidi kwa jamii wanayoihudumia.
Chanzo: Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment