Home » » WAZAZI TABORA WACHEKELEA VIBOKO KURUDISHWA SHULENI

WAZAZI TABORA WACHEKELEA VIBOKO KURUDISHWA SHULENI

Jumuia ya Umoja Wazazi Tanzania wametakiwa kuishauri serikali kusimama katika nia yake ya kurejesha adhabu ya viboko mashuleni ili kuboresha nidhamu kwa wanafunzi ambayo imekuwa ikimomoyoka siku hadi siku.

Mwenyekiti wa Chama cha mapinduzi (CCM) wilaya ya Tabora Bw, Moshi Omary, ameitaka jumuia ya wazazi hapa nchini kuindikia barua rasmi ya kuiomba serikali iweke mkazo katika kurejesha  adhabu ya viboko shuleni.

Bw, Omary amesema kuwa hatua hiyo itasaidia kukuza nidhamu shuleni na kupunguza vitendo vya kihuni miongoni mwa wanafuni.

Kwa upande wake mjumbe wa baraza kuu la wazazi Taifa Bw. Kajoro Vyohoroka, Amekitaka Chama cha (CCM) kutoa nafasi sawa za uwakilishi kwa jumuia zake katika nafasi za maamuzi kama ujumbe wa Nec na Ubunge.

Mjumbe huyu wa jumuia hiyo amesema ccm imetoa nafasi nyingi za ujumbe wa Nec na Ubunge kwa jumuia za vijana na wanawake na kuisahau jumuia hiyo.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa