Home » » Mrundi anaswa akisafirisha watoto

Mrundi anaswa akisafirisha watoto



na Thomas Murugwa, Tabora

MAOFISA wa Uhamiaji mkoani Tabora wanamshikilia raia wa Burundi kwa tuhuma za kuwasafirisha watoto saba kwa lengo la kuwafanyia biashara.

Ofisa Uhamiaji wa Mkoa wa Tabora, Danson Mwakipesile, alimtaja mtu huyo kuwa ni Emmanuel John (22) ambaye pia ni raia wa Rwanda.

Alisema mtu huyo alikamatwa eneo la Ulyankulu, Wilaya ya Kaliua, akiwa na watoto hao saba wenye umri kati ya miaka 12 na 14 ambao nao pia ni raia wa nchi nchi hizo.

“Tulimkamata akiwa hana vibali akiwa na watoto saba kutoka nchi jirani wakiwa na umri usiozidi miaka 14,” alisema.

Mwakipesile alisema watoto hao watatumika kama mashahidi pindi mtu huyo atakapofikishwa mahakamani.

Aliwataja watoto hao waliokuwa wakisafirishwa kuwa ni Ndayisenga Batiliza, Ndakusenga Emmanuel, Nimbonajile Nagenda, Yazid John, James Justus na Samson Banteze.

Mwakipesile alisema mtu huyo atafunguliwa mashtaka ya kuingia nchini isivyo halali na kufanya biashara ya binadamu.

Alisema hivi sasa wameweza kudhibiti wimbi kubwa la wahamiaji, lakini wanaoleta usumbufu ni wakulima wa zao la tumbaku ambao hupenda kuwatumia watoto wadogo kwenye kilimo huku wakiwalipa ujira kidogo.

Wakizungumzia kuletwa kwao nchini, watoto hao walidai waliambiwa na mtu huyo kuwa anawaleta kwa lengo la kufanya kazi kwa mshahara wa sh kati ya 30,000 hadi sh 50,000
 
Chanzo: Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa