Home » » TFDA yateketeza bidhaa hafifu

TFDA yateketeza bidhaa hafifu

MAMLAKA ya Chakula na Dawa Nchini (TFDA) Kanda ya Magharibi na Kati, imeteketeza bidhaa zisizofaa kwa matumizi ya binadamu, zenye thamani ya sh milioni 3.2.
Uteketezaji bidhaa hizo ulifanyika mkoani hapa baada ya kufanyika ukaguzi maalumu kwa wiki mbili kwenye maduka ya dawa, majengo, bohari ya dawa na maeneo mengine muhimu.
Akizungumza na waandishi wa habari eneo la kuteketeza bidhaa hizo, Mkaguzi Kanda ya Kati na Magharibi, Abel Deule, alisema ukaguzi huo ulihusisha wataalamu kutoka ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tabora na Halmashauri ya Manispaa ya Tabora na ukaguzi huo ulihusisha biashara ya chakula, dawa, vipodozi na vifaa tiba.
Deule aliongeza majengo 192 yalikaguliwa ili kuthibitisha usafi wake, usajili na vibali vya kufanyia biashara vinavyotolewa na TFDA.
Aliongeza kuwa ukaguzi huo pia ulijikita zaidi kuangalia ubora wa bidhaa za chakula, dawa, vipodozi, vifaa tiba uwepo vifaa bandia zenye viwango duni na uwepo vipodozi vyenye viambata vyenye sumu.
Deule alibainisha kuwa katika ukaguzi huo wamebaini kuwa licha ya wafanyabiashara hao kuwa na uelewa, bado wamekuwa wakiuza vipodozi vyenye viambata vyenye sumu vilivyozuiliwa kuuzwa na kutumika nchini kwa mujibu wa kifungu namba 88 (a) cha sheria ya chakula, dawa na vipodozi namba 1 ya mwaka 2003.
Alisema bidhaa zilizokamatwa na kuteketezwa ni chakula tani 0.129 cha thamani ya sh 775,000, vipodozi vilivyoisha muda wa matumizi na vyenye viambato vyenye sumu tani 0.245 vya thamani ya sh 2,298,400 na dawa za binadamu tani 0.001 zenye thamani ya sh 158,000.
Katika ukaguzi huo, yalipatikana maziwa bandia ya watoto  aina ya Lactogen namba 1 na 2 na NAN ambayo ni bandia, dawa ya chanjo ya mifugo ya Newcastle (1-2) iliyositishwa kuuzwa, dawa bandia aina ya Doxycycline Capsules gramu 100, na pombe kali iitwayo Shujaa gin ambayo haijapata usajili toka mamlaka ya chakula na dawa.MAMLAKA ya Chakula na Dawa Nchini (TFDA) Kanda ya Magharibi na Kati, imeteketeza bidhaa zisizofaa kwa matumizi ya binadamu, zenye thamani ya sh milioni 3.2.
Uteketezaji bidhaa hizo ulifanyika mkoani hapa baada ya kufanyika ukaguzi maalumu kwa wiki mbili kwenye maduka ya dawa, majengo, bohari ya dawa na maeneo mengine muhimu.
Akizungumza na waandishi wa habari eneo la kuteketeza bidhaa hizo, Mkaguzi Kanda ya Kati na Magharibi, Abel Deule, alisema ukaguzi huo ulihusisha wataalamu kutoka ofisi ya Mganga Mkuu wa Mkoa wa Tabora na Halmashauri ya Manispaa ya Tabora na ukaguzi huo ulihusisha biashara ya chakula, dawa, vipodozi na vifaa tiba.
Deule aliongeza majengo 192 yalikaguliwa ili kuthibitisha usafi wake, usajili na vibali vya kufanyia biashara vinavyotolewa na TFDA.
Aliongeza kuwa ukaguzi huo pia ulijikita zaidi kuangalia ubora wa bidhaa za chakula, dawa, vipodozi, vifaa tiba uwepo vifaa bandia zenye viwango duni na uwepo vipodozi vyenye viambata vyenye sumu.
Deule alibainisha kuwa katika ukaguzi huo wamebaini kuwa licha ya wafanyabiashara hao kuwa na uelewa, bado wamekuwa wakiuza vipodozi vyenye viambata vyenye sumu vilivyozuiliwa kuuzwa na kutumika nchini kwa mujibu wa kifungu namba 88 (a) cha sheria ya chakula, dawa na vipodozi namba 1 ya mwaka 2003.
Alisema bidhaa zilizokamatwa na kuteketezwa ni chakula tani 0.129 cha thamani ya sh 775,000, vipodozi vilivyoisha muda wa matumizi na vyenye viambato vyenye sumu tani 0.245 vya thamani ya sh 2,298,400 na dawa za binadamu tani 0.001 zenye thamani ya sh 158,000.
Katika ukaguzi huo, yalipatikana maziwa bandia ya watoto  aina ya Lactogen namba 1 na 2 na NAN ambayo ni bandia, dawa ya chanjo ya mifugo ya Newcastle (1-2) iliyositishwa kuuzwa, dawa bandia aina ya Doxycycline Capsules gramu 100, na pombe kali iitwayo Shujaa gin ambayo haijapata usajili toka mamlaka ya chakula na dawa.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa