Home » » Wananchi wahimizwa kupanda Miti

Wananchi wahimizwa kupanda Miti

WANANCHI Wilayani Urambo wamehimizwa kupanda miti kwa wingi ili kutunza mazingira kwa vile zao la tumbaku linatumia kuni nyingi.

Akizindua hifadhi ya Misitu ya Halmashauri ya wilaya ya Urambo, Kiongozi wa mbio za mwenge wa Uhuru, Juma All Simai,amesema kutokana na zao la tumbaku kutumia sana kuni kukaushia tumbaku ni lazima wananchi wawe mstari wa mbele kupanda miti kwa wingi na kutunza mazingira.

Amesema kama wasipotunza mazingira kwa kupanda miti,watakabiliwa na jangwa lakini pia kukosa nishati ya kukaushia tumbaku yao.

Akiweka jiwe la mingi Shule ya Msingi ya Santa Maria,Kiongozi huyo amepongeza uwekezaji katika elimu na hasa mipango ya uongozi wa shule hiyo baadae kuwa na Chuo cha ualimu,akisema itasaidia kupunguza zaidi tatizo la walimu wilayani Urambo.

Awali Mkurugenzi wa Shule hiyo,Emmanuel Soko,alisema mipango ya shule yake ni kutoa elimu bora kuanzia shule ya msingi,sekondari na baadae Chuo cha Ualimu ili vijana watakaokuwa wanamaliza shuleni hapo wanaopenda kuwa walimu wajiunge na kufundisha katika mazingira waliyokulia na kuyazoea.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa