Home » » Watendaji wasioitisha vikao vya taarifa ya matumizi na mapato kunyimwa pesa

Watendaji wasioitisha vikao vya taarifa ya matumizi na mapato kunyimwa pesa

WATENDAJI wa Vijiji na Kata wilayani uyui, wameonywa kuwa kama hawataitisha vikao vya kueleza taarifa za mapato na matumizi,hawataruhusiwa kutumia pesa.

Akifungua mafunzo elekezi kwa watendaji wa Kata,Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Tabora,Uyuni Said Ntahondi amesema kuanzia sasa hilo litazingatiwa na pia hatua za kinidhamu zitachukuliwa dhidi yao.

Amebainisha kwamba vikao vya kutoa taarifa za mapato na matumizi ni muhimu kwa vile vinarudisha imani ya wananchi katika kuchangia miradi ya maendeleo.

Kwa upande wao watendaji hao wameeleza ili waweze kutimiza majukumu yao kikamilifu ni lazima wawezeshwe kwa vitendea kazi kwa vile wanakabiliwa na changamoto nyingi zinazowakwamisha katika utendaji wao wa kazi.

Naye afisa utumishi wa Halmashauri hiyo Ahmada Suleiman amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwawezesha watendaji hao wa Kata watekeleze majukumu yao kikamilifu na sio kufanya kazi kwa mazoea.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa