Home » » Wauguzi waaswa kutotumia mgomo kudai maslahi yao

Wauguzi waaswa kutotumia mgomo kudai maslahi yao



WAUGUZI nchini wameaswa kutotumia migomo kama silaha yao ya kudai maslahi kutoka serikali badala yake watumie mazungumzo kupitia chama chao.

Hayo yameelezwa na Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii,Dk.Hussein Mwinyi katika Hotuba yake iliyosomwa na mkuu wa wilaya ya Tabora,Bw.Suleiman Kumchaya katika ufunguzi wa mkutano Mkuu wa wauguzi Nchini,TANNA,unaofanyika mjini Tabora.

Amesema serikali inatambua kazi nzuri inayofanywa na wauguzi Nchini na kuwasihi waendelee kutoa huduma bora kwa wagonjwa wakati Serikali ikiendelea kushughulikia maslahi yao.

Dk.Mwinyi amewahakikishia wauguzi Nchini kuwa kuanzia mwaka ujao wa fedha wataanza kupewa posho ya shilingi laki tatu kwa kila mtumishi kwa ajili ya sare kila mwaka.

Awali Mganga mkuu wa Mkoa wa Tabora,Dk.Leslie Mhina amesema endapo matatizo ya wauguzi yakitatuliwa ina maana kuwa zaidi ya asilimia sabini ya matatizo katika sekta ya Afya yatakuwa yametatuliwa.

katika Risala yao wauguzi wameitaka serikali pamoja na mambo mengi kuwapatia mikopo ya nyumba na vyombo vya usafiri pasipo riba,wakitaka kulipwa ya kama madaktari wanapoitwa kufanya kazi kwa dharula na kuwa na kurugenzi ya uuguzi na sio kitengo.

Mkutano huo wa siku tatu unahudhuriwa na wauguzi zaidi ya elfu moja kutoka Mikoa yote Tanzania bara huku kauli mbiu yao ikiwa ni kuziba pengo kufikia malengo ya Milenia.


0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa