Home » » Serikali kuwachukulia hatua wanaojenga juu ya mabomba

Serikali kuwachukulia hatua wanaojenga juu ya mabomba

SERIKALI Mkoani Tabora itawachukulia hatua wananchi waliojenga juu ya miundombinu ya maji kama mabomba ili kuepusha hasara kwa wananchi wengi.

Kauli hiyo imetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Tabora,Bi Fatma Mwassa,katika hotuba yake iliyosomwa na mkuuwa wilaya ya Tabora,Bw.Suleiman kumchaya,wakati wa uzinduzi wa Bodi mpya ya mamlaka ya majisafi na taka,TUWASA,Manispaa ya Tabora..

Amesema itakuwa ni jambo la ajabu endapo watu waliojenga juu ya mabomba kuachwa pasipo kuchukuliwa hataa zozote kwani wanahatarisha upatikanaji wa maji kwa walio wengi.

Akizungumzia watu waofanya uharibifu kwenye vyanzo vya maji,Mkuu wa mkoa amesema nao watashughulikiwa kwa vile wanahatarisha upatikanaji wa maji ambao ni uhai wa wananchi.

Amesema ni lazima vyanzo vya maji vilindwe kwa kuhakikisha vinakuwa salama ili wananchi wasitishiwe uhai wao kwa kukosa huduma ya maji ambayo ni muhimu kwa uhai wao.

Kwa upande wake mwenyekiti wa Bodi ya TUWASA iliyomaliza muda wake,Mchungaji mstaafu Paulo Misigalo,amesema bodi yake imefanya kazi nzuri ikiwemo kuongeza mapato ya Mamlaka kutoka shilingi milioni 150 hadi shilingi milioni 230 kwa mwezi na kuifanya mamlaka kupata hati safi toka Mdhibiti na mkagzui mkuu wa serikali,CAG.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa