Home » » ZIARA YA ZITTO KABWE KANDA YA MAGHARIBI,JIMBO LA IGALULA

ZIARA YA ZITTO KABWE KANDA YA MAGHARIBI,JIMBO LA IGALULA

Siku ya 5 ya ziara ya CHADEMA Kanda ya Magharibi imetufikisha Jimbo la Igalula, wilaya ya Uyui. Tumekutana na wananchi katika vijiji vya  Goweko, Loya, Miswaki, Miyenze na Kigwa.
Tumezungumza kuhusu  changamoto ya usafiri wa Reli, wafugaji kunyanyaswa na watendaji wa kata na askari kwa kunyanganywa mifugo, zao la Tumbaku, maji safi na salama  na suala la jumla la Katiba na mchakato wa kuandika katiba. 
Kimsingi shughuli za kiuchumi za wananchi ni kubwa na hasa Kilimo na  mifugo. Hata hivyo ukosefu wa miundombinu unafanya wananchi wasipate  thamani ya mazao yao na jasho la kazi zao. 
Nilipofika Kijiji cha Loya nimeona eneo kubwa lina miti ya mihama.  Wananchi wanatumia tu mihama wakati wa njaa na mara nyingi matunda haya  yanaharibika tu. Lazima matunda haya yana matumizi yake ya kiviwanda  maana ‘kernel’ yake ina mafuta.  Na hili ni swali aliloacha Mh Zitto Kabwe Nani anajua matumizi ya Mihama?

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa