Home » » HALMASHAURI YAOMBA BAJETI YA BIL.35

HALMASHAURI YAOMBA BAJETI YA BIL.35

BARAZA la madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Nzega mkoani Tabora limeomba kuidhinishiwa kiasi cha sh 35,455,837,199 kwa mwaka wa fedha wa 2014/2015.
Akisoma taarifa ya bajeti hiyo, Kaimu Ofisa Mipango wa halmashauri hiyo, Martin Jakanyango, alisema kiasi hicho kinajumuisha sh 1,378,203,500 kama vyanzo vya ndani vya halmashauri.
Jakanyango alitaja kuwa ruzuku ya fidia ya kodi waliyopanga ni sh 579,594,000, ruzuku kutoka Serikali Kuu kwa ajili ya mishahara ni sh 23,978,711,716.
Alitaja ruzuku kwa ajili ya matumizi ya kawaida ni sh 2,911,348,000, ruzuku kwa ajili ya miradi ya maendeleo ni sh 5,326,293,982, ruzuku kwa ajili ya mifuko ya pamoja ni sh 1,231,686,001 huku michango ya wahisani ikiwa sh 50,000,000.
Katika kikao hicho, baraza hilo lilipitisha bajeti ya halmashauri ya mji mdogo wa Nzega kiasi cha sh 1,012,372,763 kwa mwaka huo wa fedha.
“Taarifa hiyo inasema kiasi cha sh 1,228,220,000 kitatokana na vyanzo vya ndani, fidia ya kodi sh 360,000,000 na ruzuku kutoka Serikali Kuu sh 807,526,190,” alisema.
Chanzo;Tanzania daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa