Home » » KITUNDA,POLISI KUPAMBANA NA UHALIFU

KITUNDA,POLISI KUPAMBANA NA UHALIFU


KAMPUNI ya uchimbaji madini ya Kitunda Gold Mining, iliyopo Wilaya ya Sikonge mkoani Tabora, imeahidi kushirikiana na Jeshi la Polisi katika kupambana na vitendo vya kihalifu kwenye msitu wa Kitunda na eneo la mgodi huo.
Mkurugenzi wa mgodi huo, Samuel Chitalilo alisema hayo hivi karibuni, alipozungumza na gazeti hili kuhusiana na mipango mikakati ya kupambana na uhalifu maeneo hayo na kwingineko.
Alisema suala la usalama kwa raia na mali zao ni jambo muhimu, linalopaswa kuungwa mkono na jamii yote, na alilipongeza Jeshi la Polisi wilayani Sikonge na Tabora kwa ujumla kwa kuanzisha operesheni maalumu ya kupambana na vitendo vya uhalifu.
“Kampuni yangu ya Kitunda Gold Mine itaendelea kushirikiana na Jeshi la Polisi kuhusu kupambana na uhalifu eneo la pori la Kitunda na maeneo ya mgodi,” alisema.
Katika hatua nyingine, Chitalilo ambaye pia ni mbunge wa zamani wa Buchosa, alisema kampuni yake hiyo inakusudia kuanza kutoa vitambulisho maalumu kwa wachimbaji wote wa mgodi huo.
Alisema vitambulisho hivyo vitachangia kwa asilimia kubwa kuwatambua vijana wanaojishughulisha na masuala ya uchimbaji madini eneo hilo, hivyo kurahisisha pia kuwachukulia hatua pale watakapobainika kujihusisha na mambo mabaya.
Chanzo;Tanzania daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa