Home » » AIRTEL YAWAPATIA MAFUNZO WAFANYAKAZI WA AFYA

AIRTEL YAWAPATIA MAFUNZO WAFANYAKAZI WA AFYA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

WAFANYAKAZI wa afya wa Kijiji cha Mbola, mkoani Tabora, wameishukuru Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel Tanzania kutokana na teknolojia ya huduma ya mawasiliano inayowawezesha kutoa huduma za afya kwa wigo mpana.
Wafanyakazi hao walipata mafunzo ya namna ya kutumia teknolojia ya huduma ya afya kupitia simu iitwayo COMCARE, iliyoanzishwa kwa msaada wa Dagiba ambayo inapatikana kupitia simu za smart phone zenye ‘application’ maalumu inayowawezesha wafanyakazi wa afya kukusanya takwimu za wagonjwa na kutuma ripoti kwenye vituo vya afya.
Akizungumza wakati wa mafunzo,  mmoja wa wafanyakazi wa afya, Amina Wakasuvi, alisema teknolojia hiyo itawawezesha kufuatilia kazi zinazofanywa na wafanyakazi wa afya katika maeneo mbalimbali na wafanyakazi hao wataweza kutuma ripoti zao kwa wakati kila siku kupitia mtandao wa Airtel.
“Tunawashukuru Airtel kwa ubunifu huu na huduma ya vifurushi vya intaneti vya bure vinavyotuwezesha kufanya kazi zetu kwa wakati,” alisema.
Meneja Huduma kwa Jamii  wa Airtel, Hawa Bayumi, alisema kwa miaka mitatu sasa Airtel imewekeza katika kuleta mapinduzi ya kupatikana kwa  huduma kwa jamii hususani katika maeno ya vijiji vya Tabora  kwa kushiriki katika mradi wa  Millennium Village kama mtoaji mkuu wa huduma za mawasiliano.
Katika mradi huo, Airtel inatoa njia ya mawasiliano kwa kuwezesha jamii inayoishi katika maeneo ya pembezoni kupata huduma za afya. Wafanyakazi wa afya katika maeneo hayo wameunganishwa na mtandao wa kisasa unaowapatia huduma ya intaneti na simu na kurahisisha kazi zao pindi wakiwa kazini.
Akizungumzia mradi huo, Mkurugenzi wa mradi wa Millennium Village, Dk. Gerson Nyadzi, alisema mtandao wa 3G wa Airtel umewawezesha kwa kiasi kikubwa  kufikia maeneo ya vijijini  ambako huduma ni duni na haba. 
Chanzo:Tanzania Daima

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa