Home » » RAGE ADAIWA KUWASALITI WABUNGE WENZAKE

RAGE ADAIWA KUWASALITI WABUNGE WENZAKE

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

MBUNGE wa Tabora Mjini, Ismail Aden Rage, anadaiwa kuwasaliti wabunge wa mkoa wa Tabora kwa kupeleka taarifa kwa waziri mkuu Mizengo Pinda, juu ya mipango ya wabunge wa mkoa huo  kuishinikiza serikali ya Chama cha Mapinduzi (CCM)kutekeleza miradi ya maendeleo ya mkoa.
Rage alidaiwa kufanya usaliti huo Katika bunge la bajeti la mwaka jana wakati wabunge wa mkoa wa Tabora walipokaa kwa pamoja na kutaka kususia bajeti ya Waziri wa Ujenzi, Dk John Magufuli, kutokana na kuendelea kusuasua kwa miradi ya maendeleo ya mkoa huo hususan miradi ya barabara.
Chanzo kutoka kwa mmoja wa wabunge wa mkoa huo, kilieleza lengo la wabunge hao ilikuwa ni kutoka nje wakati wa kusomwa kwa bajeti ya wizara ya ujenzi 2013/2014, ili  kuonyesha namna serikali ya CCM ilivyoshindwa kuthamini uzalendo wa wananchi wa mkoa wa Tabora
“Tulikaa kwa pamoja tukajiuliza kosa letu Tabora ni kuwa na majimbo yote yanayoongozwa na CCM ama unyonge wetu wa kushindwa kupigania maslahi ya wananchi kwa ajili ya kukilinda chama..tukasema hapana lazima sasa tuonyeshe kukerwa kwetu na njia nzuri tulichagua kususia bajeti ya Wizara ya Ujenzi,” kilieleza chanzo chetu.
Alisema muda mfupi kabla ya bajeti ya wizara hiyo haijasomwa, wabunge wa Tabora wanaotokana na CCM waliitwa katika kikao cha dharura kwa kupigiwa simu na Waziri Mkuu Pinda, kwa ajili ya kutafuta muafaka.
Alisema katika kikao hicho ndipo walipobaini Waziri Mkuu alifikishiwa taarifa na Rage, hali iliyomfanya mmoja wa wabunge wa viti maalum kuangusha kilio.
Alipoulizwa kuhusu suala hilo, Mbunge wa Sikonge, Said Nkumba,  alikiri kukutana na Waziri Mkuu pamoja na Naibu Waziri wa Uchukuzi kwa wakati huo na kusema kuwa kikao hicho hakikuitishwa na Waziri Mkuu huku akikanusha mpango wa wabunge kutaka kususia bajeti ya Wizara ya Ujenzi
Alisema baada ya kikao hicho baadhi ya mambo yalishughulilikiwa na kwamba katika bajeti ya mwaka huu barabara ya Sikonge-Mpanda imetengewa fedha kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wake
Kwa upande wake Rage alipoulizwa alikana mwaka jana wabunge wa mkoa huo hawakukaa kikao chochote na Waziri Mkuu kwa ajili ya kujadili kusuasua kwa maendeleo ya mkoa wa Tabora.
Chanzo;Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa