Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
DIWANI wa Ipuli, Waziri Mlenda, amemtaka Mkuu wa Wilaya, Suleimani
Kumchaya, asiingilie masuala ya ugawaji wa viwanja katika kata hiyo
kwani anatakiwa afuate taratibu, sheria na kanuni za ugawaji viwanja.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake juzi, alisema
Kumchaya sio kazi yake ya kusimamia mgogoro wa viwanja, na hapaswi
kulazimisha halmashauri igawe viwanja kwa wananchi.
‘Mimi ni Diwani wa Ipuli, nasema kutopewa nafasi ya kuzungumza na
wananchi kwenye mkutano wa hadhara katika kata yangu hiyo ni kunijengea
sifa mbaya kwa wananchi.
“Mkuu wa wilaya anapaswa atoe mawazo ya kuwajenga wananchi na sio
kuiponda kamati ya Uongozi na kuichafua kwa kuwalainisha wananchi kwa
maneno ambayo hayahusiki katika mikutano inayofanyika katika kata hii,”
alisema.
Alisema katika ugawaji huyo Mkuu wa Wilaya anatakiwa kuangalia kwa
makini kuna wananchi 1,136 na viwanja vinavyopimwa ni 646 kwa mpangilio
huo itakuwa mgumu kutokana na viwanja kuwa vichache na wananchi kuwa
wengi.
Alitoa wito wa wananchi wa Ipuli kuwa wavumilivu katika ugawaji wa
viwanja kama walivyozungumza kwenye mkutano uliopita kabla hajafika
Mkuu wa Wilaya huyo katika mkoa huo
Chanzo:Tanzania Daima
0 comments:
Post a Comment