Home » » MAAMBUKIZI YA VVU KWA WAJAWAZITO YAPUNGUA

MAAMBUKIZI YA VVU KWA WAJAWAZITO YAPUNGUA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
MAAMBUKIZI ya virusi vya ukimwi (VVU) kwa wajawazito yamepungua kutoka asilimia 3 hadi 2.3.
Hayo yamebainishwa na Meneja wa shirika lisilo la kiserikali la EGPAF Mkoa wa Tabora, Alphaxard Lwitakubi, alipozungumza na waandishi wa habari na kueleza kuwa wajawazito walioweka wazi hali zao ni asilimia 63.
Alisema kati ya walioweka hali zao wazi wapo waliopatiwa dawa za kuzuia maambukizi ya VVU toka kwa mama kwenda kwa mtoto.
Akizungumzia changamoto wanazokabiliana nazo, Lwitakubi alisema ni kukosa ushirikiano upande wa wanaume katika masuala ya afya ya uzazi na upimaji VVU.
Changamoto nyingine aliyoitaja ni wajawazito kujifungulia nyumbani, waliogundulika na maambukizi kutorudi vituoni, walezi na wazazi kutopeleka watoto walioathirika katika vituo vya afya
Chanzo:Tanzania Daima 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa