Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
RAIS
Jakaya Kikwete, amewashauri mawakala wanaouza mashine za risiti za
kielektroniki (EFDs) kuwaongezea muda wafanyabiashara wa kulipa gharama
za mashine hizo ili kuondoa malalamiko ya gharama kubwa za mashine hizo.
Aidha,Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imemshukuru Rais Kikwete kwa kuwasaidia kuhamasisha matumizi ya mashine hizo.
Akiwa katika siku ya
pili ya kutembelea Maonesho ya 38 ya Biashara ya Kimataifa yaliyofikia
kilele chake jana katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere, Rais
alipongeza kazi zinazofanywa na mamlaka hiyo.
Akiwa kwa mawakala
wanaouza mashine hizo za EFds, Rais alisema kutokana na malalamiko ya
wafanyabiashara kuhusu gharama za mashine hizo ni vema kuwaongezea muda
wa kulipa.
"Kama ni suala la bei
kubwa, wapeni muda mrefu wa kulipia mashine hizo na kama wataendelea
kulalamika huyo atakuwa na lake,"alisema Rais.
Akiwa katika banda hilo
la TRA, alipokewa na Kamishna Mkuu wa TRA, Rishad Bade ambaye
alimweleza kazi wanazofanya ikiwemo uanzishaji wa mifumo miwili mipya ya
usafirishaji mizigo nje ya nchi.
Bade alisema, mfumo huo
wa forodha uliounganishwa na TANCIS utasaidia katika kudhibiti upotevu
wa mizigo na nyaraka mbalimbali katika nchi za Jumui ya Afrika
Mashariki.
Akiwa katika banda
hilo,Rais Kikwete alifurahia uanzishwaji wa vilabu mbalimbali vya kodi
katika shule za sekondari kwa nia ya kuwajengea vijana moyo wa kulipa
kodi.
Mara baada ya ziara ya Rais, Bade alimshukuru Rais kwa kuhamasisha jamii kutumia mashine za EFDs jambo lililofanya suala hilo kuwa rahisi na wananchi kuitikia kwa nguvu.
Alisema, katika
maonesho hayo TRA wameshika nafasi ya pili kwa taasisi za serikali huku
akiweka bayana kuwa mifumo mipya miwili waliyoanza kutumia Julai Mosi,
mwaka huu itarahisisha ufanisi katika huduma zao za ukusanyaji mapato.
Katika ziara hiyo, Rais
Kikwete alianza kwa kutembelea Banda la Mamlaka ya Elimu ya Ufundi
(VETA) ambapo alifurahia ugunduzi wa bidhaa mbalimbali na kutaka ubunifu
huo kuendelea zaidi.
Alipofika katika
kitanda kilichotengenezwa kwa mchanganyiko wa mbao za msufi na
nyinginezo aliwataka kutumia miti hiyo iliyoko mingi katika maeneo
mbalimbali nchini.
Rais Kikwete pia
alitembelea mabanda mengineya Jeshi la Kujenga Taifa (JKT),Kampuni ya
Simu (TTCL)Shirika la Hifadhi za Jamii la PPF,Chuo Kikuu cha Ardhi,Jeshi
la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
Katika mabanda hayo
alipongeza juhudi wanazofanya za utoaji huduma na kutaka kuongeza
uwajibikaji ikiwa ni pamoja na kuongeza ubunifu katika huduma zao.
Chanzo:Majira
0 comments:
Post a Comment