Home » » WAJASIRIAMALI WAKOPESHWAMILIONI 100.4/-

WAJASIRIAMALI WAKOPESHWAMILIONI 100.4/-

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
 

JUMLA ya sh.100,400,000 zimekopeshwa kwa wajasiriamali wapatao 974 mkoani Tabora kwa lengo la kuondoa umaskini na kuongeza ajira kwa wananchi.

Hayo yamebainishwa na Meneja wa Shirika la kuhudumia viwanda vidogo (SIDO) Mkoa wa Tabora Samwel Neligwa ofisini kwake alipokuwa akizungumza na mwandishi wa gazeti hili.

Alisema ili kufikia lengo la shirika hilo la kuondoa umaskini pamoja na kukuza maendeleo ya viwanda vidogo vidogo na biashara alisema SIDO imeweza kutoa mikopo hiyo kwa wajasiriamali wa mkoa huo na hivyo kuongeza ajira 1,637.

Alisema katika kipindi cha mwaka 2009/10 hadi 2013/14 mafunzo mbalimbali 228 yalitolewa kwa wajasiriamali wapatao 4,485.

Alieleza mkakati mwingine unaofanywa na SIDO kuwa ni kuibua na kuendeleza bidhaa maalum katika kila wilaya kwa kuzingatia malighafi na utaalam uliopo kwenye wilaya husika.

Neligwa alisema lengo la mkakati huo ni kuweza kuhamasisha wilaya husika kuchagua bidhaa maalum itakayoweza kusaidia kuharakisha maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi.

Alisema uhamasishaji huo hufanywa kwa kushirikiana na ofisi za wilaya na utekelezaji wake hufanywa kwa kuunganisha nguvu na rasilimali zilizopo za SIDO na serikali.

Aliyataja mazao yanayopewa msukumo mkubwa katika mkakati huo unaofanyika katika wilaya zote za Mkoa wa Tabora kuwa ni asali na nta, alizeti, mpunga, viatu na bidhaa mbalimbali za ngozi.

Neligwa ameeleza kuwa mkakati huo unaojulikana kwa jina la wilaya moja bidhaa moja (ODOP) alisema umetoa fursa kubwa kwa vijana vijijini ambako ndiko walipo vijana wengi kuweza kujiajiri kutokana na kuanzisha miradi na viwanda vidogo na hivyo kusema hali hiyo imeweza kuleta matokeo makubwa kiuchumi na kuongeza kipato na ajira kwa vijana.

Aliongeza kusema kuwa hivi sasa tayari kuna wajasiriamali wa bidhaa za ngozi ambao baada ya kuwezeshwa na SIDO wajasiriamali hao uzalishaji wao umeongezeka na hata kufungua maduka ya viatu vya ngozi.

Alisema licha ya wajasiriamali hao kuweza kujiajiri wenyewe lakini wameweza kuajiri pia watu wengine baada ya kufungua maduka ambayo yapo Tabora mjini na Igunga.

Neligwa alisema katika programu ya kusaidia mafundi wanashirikiana na shirika lisilo la kiserikali la Uingereza lijulikanalo kama TOOLS FOR SELFRELIANCE

Chanzo:Majira

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa