Home » » TABORA YAANDIKISHA 53,581 ELIMU YA AWALI.

TABORA YAANDIKISHA 53,581 ELIMU YA AWALI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 

MKOA wa Tabora umeandikisha jumla ya watoto 53,581 wa elimu ya awali katika mwaka wa masomo 2016.
Hayo yalibainishwa na Katibu Tawala Msaidizi anayeshughulikia elimu mkoani Tabora, Juma Mhina. Alitoa taarifa hiyo katika kikao cha wadau wa elimu cha hivi karibuni, kilichoshirikisha maofisa kutoka halmashauri zote saba za mkoa huo.

Alisema idadi hiyo ni ya watoto wote walioandikishwa katika halmashauri zote za mkoa huo. Idadi halisi ya watoto waliotarajiwa kuandikishwa ni 74,773 .

Alisema wavulana walioandikishwa ni 21,664, sawa na asilimia 57.6 na wasichana ni 21,917 sawa na asilimia 58.9.
Jumla ya watoto wote walioandikishwa katika wilaya zote ni 53,581, sawa na asilimia 71.6. Halmashauri ya Manispaa ya Tabora imefanikiwa kuvuka lengo la makisio yake, ambapo watoto waliotarajiwa kuandikishwa ni 4,881, lakini walioandikishwa ni 5,099 sawa na asilimia 104.5.

Akizungumzia uandikishwaji watoto wa kuanza darasa la kwanza, Mhina alisema mkoa huo umefanikiwa kuandikisha jumla ya watoto 64,642 sawa na asilimia 70.6 wakati matarajio ilikuwa kuandikisha watoto 91,506.

Alipongeza halmashauri ya Manispaa Tabora kwa kufanikiwa kuvuka lengo la uandikishaji, ambapo iliandikisha watoto 7,644 sawa na asilimia 110 wakati matarajio yalikuwa kuandikisha watoto 6,924.
CHANZO: HABARI LEO.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa