Home » » TEMESA YASISITIZA SHERIA ZIFUATWE KUTENGENEZA MAGARI YA SERIKALI.

TEMESA YASISITIZA SHERIA ZIFUATWE KUTENGENEZA MAGARI YA SERIKALI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
Imeandikwa na Raymond Mushumbusi,




WAKALA wa Ufundi na Umeme (Temesa) imewazuia wamiliki na waendeshaji wa karakana teule zilizopewa mamlaka na wakala huo kutengeneza magari na vifaa vya Serikali, kutofanya matengenezo ya magari na vifaa hivyo bila kufuata utaratibu wa wakala.
Akizungumza katika kikao kati ya Temesa, wamiliki na waendeshaji wa karakana teule, Kaimu Mtendaji Mkuu wa Temesa, Manase Lekujan alisema, karakana teule zinatakiwa kufuata taratibu husika kufanya matengenezo ya magari na vifaa vya Serikali.
“Tumeitisha kikao hiki na wamiliki wa karakana teule tunazofanya nazo kazi ili tukumbushane kuhusu kufanya kazi kwa kuzingatia sheria na taratibu zilizopo kwenye mikataba yetu.
Hii ni katika kuweka mpango mzuri wa kuwa na taarifa sahihi za matengenezo ya magari na vifaa vya Serikali katika karakana zetu ili kuondokana na changamoto zilizopo na kuongeza ufanisi wa kazi zetu,” alisema Manase.
Akifafanua kuhusu Sheria ya Manunuzi ya mwaka 2011, Mwanasheria wa Temesa, Gratian Mali alisema, sheria inatoa nafasi kwa Wakala huo kutafuta karakana binafsi kusaidia shughuli za matengenezo ya magari na vifaa vya Serikali pale ambapo karakana za wakala zinakuwa na kazi nyingi au kukosa baadhi ya vifaa kwa ajili ya matengenezo na kazi hizo hutolewa kwa vibali maalumu kutoka Temesa.
Akizungumza baada ya kikao hicho, mmoja wa wamiliki wa karakana ya Nduvin Auto Works, Masoud Msangi, alisema kikao kimekuwa cha mafanikio kwani imefika wakati kwa karakana teule kutekeleza agizo la kutengeneza magari na vifaa vya Serikali kwa kufuata sheria na taratibu na sio kufanya shughuli zake kiholela.
CHANZO: HABARI LEO

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa