Home » » HALMASHAURI, WAKAGUZI LAWAMANI UFAULU DUNI TABORA.

HALMASHAURI, WAKAGUZI LAWAMANI UFAULU DUNI TABORA.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
MKOA wa Tabora umeshika nafasi ya mwisho katika matokeo ya wanafunzi waliohitimu elimu ya msingi kwa mwaka jana, hali inayoonesha kushindwa kwa wahusika wa elimu kufikia malengo waliyojiwekea kuhakikisha ufaulu unapanda.
Inaelezwa kuwa, viongozi wa elimu mkoani hapa walikaa Januari 29, mwaka jana kujadili mikakati ya kupandisha ufaulu kwa shule za msingi kwenye mkoa huo, jambo lililoshindwa kuonesha mafanikio chanya katika matokeo ya wanafunzi waliomaliza shule ya msingi mwaka huo.
Mkuu wa Mkoa, Ludovick Mwananzila alisema, ana imani kuwa yaliyoazimiwa katika kikao hicho hayakufanyiwa kazi kikamilifu ndio maana mkoa huo umeshika nafasi ya mwisho Tanzania Bara, katika matokeo ya shule ya msingi.
“Nilijiuliza maswali mengi sana baada ya kupata matokeo, kulikuwa na sababu gani ya kuitisha mkutano wa wadau na kuweka maazimio lukuki kwa lengo la kuinua kiwango cha elimu na kuongeza ufaulu wa watoto wetu, inaonesha kuna maazimio hayakufanyiwa kazi ipasavyo,” alisema.
Aidha, alibainisha kuwa kitendo cha mkoa huo kufanya vibaya katika matokeo hayo kimechangiwa na Halmashauri za mkoa huo kushindwa kufanyia kazi maelekezo yaliyotolewa katika vikao husika, ikiwemo kutosimamia vizuri elimu. Aidha, aliwalaumu wakaguzi wa shule kushindwa kufanya kazi yao ipasavyo ikiwa ni pamoja na kushindwa kufuatilia endapo walimu wanafundisha au la.
CHANZO : HABARI LEO.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa