Home » » WANA CCM WATAKIWA KUFANYA KAZI SI KAMPENI.

WANA CCM WATAKIWA KUFANYA KAZI SI KAMPENI.

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399. 
CHAMA Cha Mapinduzi (CCM) Mkoa wa Tabora kimewataka viongozi wake kufanya kazi za chama na kuacha kufanya kampeni za kuelekea uchaguzi wa ndani utakaofanyika mwaka 2017.
Mwenyekiti wa CCM Mkoa, Hassani Wakasuvi alisema hayo katika uzinduzi wa sherehe za kuzaliwa kwa chama hicho zilizofanyika katika Kijiji cha Busondo, Kata ya Puge Wilaya ya Nzega, kuwa baadhi ya viongozi wameacha kufanya kazi za chama na kujikita kufanya kampeni za uchaguzi.
Akitaja ngazi za nafasi ambazo zinahangaika kufanya kampeni ni pamoja na nafasi ya balozi wa nyumba kumi, mwenyekiti wa matawi, wenyeviti wa kata, wenyeviti wa wilaya pamoja na yeye mwenyewe kwa nafasi yake wanapaswa kufanya kazi kwani muda wa uchaguzi haujafika.
Alisema baadhi ya viongozi wameanza kuwa na hofu ya kuendelea na nafasi zao, lakini wanapaswa kujikita kufanya kazi za chama bila kuegemea upande wowote ili kuepusha makundi yanayoweza kukigharimu chama hicho.
CHANZO : HABARI LEO.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa