Home » » NAIBU WAZIRI MPINA AIADHIBU MANISPAA YA MJI WA TABORA

NAIBU WAZIRI MPINA AIADHIBU MANISPAA YA MJI WA TABORA

Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazngira Mhe. Luhaga Mpina akiongea na maafisa na waaandishi wa habari alotangulizana nao katika DAMPO la mji wa Tabora na kushangazwa na hali halisi ya DAMPO hiyo na taarifa ya mazingira aliyopewa na mkoa kuhusu usafi wa mazingira wa mji wa Tabora

Bw. Benjamini Dotto Afisa Mazingira kutoka Baraza la Taifa la hifadhi na usimamizi wa mazingira NEMC (katikati) akieleza kitaalam nini kifanyike katika DAMPO la Mji wa Tabora kabla ya manispaa kuwasilisha mpango mkakati kuhusu dampo la mji huo. (Picha na Evelyn Mkokoi)


Kupitia Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) Naibu Waziri Ofisi ya Makamu wa Rais Mungano na Mazingira Mhe. Luhaga Mpina ameipa adhabu Halmashauri ya Maispaa ya Mji wa Tabora kwa kuitoza faini ya shilingi Milioni kumi na mbili na kutakiwa kulipa faini hiyo kwa muda wa wiki mbili, kwa kile kilichodaiwa ni kutokutii mamlaka za juu na kusema uwongo kuhusu hali ya usafi wa maingira ya mji wa Tabora.
Alipokoukuwa katika siku ya Pili ya ziara yake mkoani Tabora baada ya kupata taarifa ya hali ya mazingira ya mkoa huo, Na kuambiwa kuwa ni ya kuridhisha na kuwa DAMPO la mji huo ambalo siyo rasmi,lipo katika hali ya kuridhisha ndipo alipoamua kjutembelea DAMPO hilo na kujioea hali ya uchafu isiyovumilika kwa taka ngumu na hatarishi, kutomwagwa katika eneo husika na kuzagaaa barababarani.
Aidha kufuatia malalamiko ya wakazi wa mji huo, Mpina halikadhalika aliktembelea soko ya mji wa Tabora na kushuhudia Dampo katikati ya soko hilo lenye taka mbichi zenye harufu kali ambayo huweza kuhatarisha maisha ya watumiaji wa soko hilo kwa kupata magonjwa ya mlipuko kama kipindu pindu.
Kwa Upande wake Mkurugenzi wa Manispaa ya Tabora Bw. Bosco Nduguru alisema ofisi yake ilikuwa na mpango wa kuhamishia soko hilo sehemu nyingine na kukubali changamoto zilijitokeza sokoni hapo na kuzifanyia kazi wakati mwenyekiti wa soko hilo bwana Bakari Mpumila alieleza kuwa kuhamishwa kwa soko hilo hakuwezi kuwa suluhisho la kudumu kutatua changamoto za usafi wa mazingira kwani dampo linalotumika katikati ya soko hilo limekuwa ni kero iliyoshindikana toka kwa uongozi uliopita na Kumshukuru Naibu Waziri Mpina kwa ziara yake kwani ana imani kuwa sasa kero hiyo imeshatapatiwa ufumbuzi wa kudumu.
Pamoja na kulipa faini hiyo manispaa pia inatakiwa kuondosha taka hizo a kumwaga kifisi cha molamu katika eneo hilo na kurekebisha mazingira ya choo sokoni hapo.

 


0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa