Home » » MUUGUZI ANAYEDAIWA KUBAKA ACHUNGUZWA

MUUGUZI ANAYEDAIWA KUBAKA ACHUNGUZWA

Ikiwa unatukio lolote au jambo lolote tuma kupitia Barua pepe yetu blogzamikoa@live.com au Whatsapp namba +255765056399.
 
Imeandikwa na Lucas Raphael, Tabora.
Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Tabora, Wilbroad Mutafungwa

POLISI mkoani Tabora inaendelea kuchunguza tukio la muuguzi wa Kituo cha Afya Kata ya Igurubi Wilaya ya Igunga mkoani Tabora, Damiana Mgaya (26), kwa tuhuma ya kumbaka binti wa miaka 18 anayeishi Kitongoji cha Mwagala B Kijiji cha Mwagala.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Wilbroad Mutafungwa alisema wameanza uchunguzi wa uhalifu uliofanywa Julai 13, mwaka huu saa 8 hadi alfajiri wakati binti huyo akimuuguza mama yake, Tatu Simbi aliyelazwa kituo hicho cha afya baada ya kushambuliwa kwa kipigo na mumewe.
Mutafungwa alisema Mgaya alimpokea mama wa binti huyo akiwa hoi na ndipo alimpatia matibabu, kisha kumlaza katika kituo hicho cha afya huku akimchoma sindano ya usingizi, ambayo ilisababisha mama huyo kupitiwa na usingizi.
Alisema muuguzi huyo alichoma binti huyo sindano ya usingizi, ndipo alimwingilia kimwili na kumsababishia maumivu makali mwili mzima. Alisema baada ya kuambiwa hivyo, binti huyo alikubali kuchomwa sindano mbili na alipochomwa sindano ya kwanza aliishiwa nguvu na alipochomwa sindano ya pili, alianguka na kupitiwa na usingizi hadi asubuhi.
Alisema baada ya kuona amelala pasipokuwa na fahamu, muuguzi huyo alianza kumbaka hadi alfajiri alipoamshwa na mama yake huku yeye akiwa hajitambui kutokana na maumivu aliyokuwa akiyasikia sehemu zake za siri na mwili wote. Alisema kwa sasa binti huyo hali yake ya afya inaendelea vizuri.
CHANZO HABARI LEO
 

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa