NA TIGANYA VINCENT
RS TABORA
10 January 2018
SERIKALI
 Mkoani Tabora imepiga marufuku uegeshaji wa malori katika maeneo yasiyo
 rasmi mjini Igunga kwa sababu yamekuwa yakivunja Sheria ya Mipango Miji
 Namba 8 ya mwaka 2007 na pia yamekuwa yakichangia uuaji miti 
iliyopandwa kando kando ya barabara kuu.
Kauli
 hiyo ilitolewa jana mjini Igunga na Mkuu wa Mkoa wa Tabora Aggrey 
Mwanri baada ya kuzindua wiki moja ya upandaji miti kando kando ya 
barabara kuu iliyokuwa ikifanywa na wanafunzi wa Shule za Msingi na 
Sekondari katika Wilaya ya Igunga na wilaya nyingine mkoani kote.
Alisema
 kuwa uegeshaji huo umekuwa ukiisababishia hasara Halmashauri hiyo 
kutokana na malengo yake ya kupanda miti kukatizwa kwa kwa sababu ya 
kufa kufuatia kukayangwa na magari yanayoegeshwa katika sehemu hizo 
zisizo rasmi.
Mwanri
 alisema kuwa lori litakalokamatwa limeegeshwa na Dereva wake katika 
sehemu ambayo haikutengwa na Halmashauri ya Igunga, mhusika atatozwa 
faini ndipo aruhusiwe kuendelea na safari yake mara baada ya mapumziko.
Alitoa
 wito kwa madereva wa malori kuwa ni vema wakaheshimu Sheria na taratibu
 zilizopo zinazowataka kuegesha magari yao katika maeneo yaliyotengwa na
 Halmashauri zote ambazo ziko njia kuu ili kuepusha uharibifu wa miti 
inayopandwa.
Mwanri
 alisema kuwa Sheria ya Miapango miji inatoa muongozo ya kupanga mji na 
sio kufanya shughuli zao na kukaa kiholela holea , hata katika maeneo 
hawakupangiwa kuaa.
Alisema
 kuwa Dereva akitaka kupumzika ni vema akapeleka gari kwanza katika eneo
 lilitengwa kwa ajili ya shughuli hiyo ndipo aende mapumziko na sio 
kuliacha kando kando ya barabara na kunyaga miti ambayo jamii na 
Halmashauri imetumia muda na fedha kuipanda.
“Hapa
 ni mjini ni lazima madereva waheshimu Sheria ya Mipango miji kwa 
kuegesha magari yao katika maeneo waliotengewa wakati wanapojisikia 
uchovu na wanahitaji kupumzika…la sivyo tutawakamata na kutoaza faini, 
sio kila eneo ni la kulaza gari” alisema Mkuu huyo wa Mkoa.
Alisema
 kuwa njia kuu ndio uso wa sehemu husika, kwa hiyo kitendo cha kuacha 
magari yanakaa na kuegeshwa ovyo ovyo barabarani hasa katika sehemu ya 
Igunga kunaharibifu sura ya Tabora.
Aidha
 Mwanri alisema kuwa atamchukulia hatua kali Kiongozi yoyote 
atakayebainika kuendesha vitendo vya kuwafanya madereva walaze malolri 
katika maeneo yasiyo rasmi kwa maslahi binafsi.
Naye
 Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Igunga Revocatus Kuuli 
alisema kuwa msimamo wao ni kuwa magari yote yanatakiwa yaegeshwe katika
 eneo maalumu lililotengwa mjini hapo kwa ajili ya kulaza magari, 
kinyume cha hapo ni kufanya kosa.
Alisema
 kuwa Dereva atakayekamatwa akiwa amelaza gari lake kando kando ya 
barabara atachukuliwa hatua yeye na mlinzi wa kulinda gari lake kwa kuwa
 tayari walishatoa maelekezo.
Aidha
 Mkurugenzi huyo Mtendaji alitoa wito kwa vijana au watu wanajifanya 
walinzi wa magari makubwa yanayoegeshwa katika sehemu isiyo rasmi kuacha
 tabia hiyo na kama wanahitaji fedha waende katika Ofisi za Halmashauri 
iwapatie kazi za kufanya au maeneo ya kufanyia kazi ili wasivunje 
Sheria.
 

 
 
 
 
 
 
 
 
 
0 comments:
Post a Comment