Home » » Mahakama Kuu yatupa Rufani ya mauaji na kubaka

Mahakama Kuu yatupa Rufani ya mauaji na kubaka


MAJAJI wa Mahakama ya Rufaa Nchini wanaoendelea na kikao  mjini Tabora wametupilia mbali Rufaa tatu zilizofunguliwa kupinga maamuzi  yaliyotolewa na Mahakama za chini kwamba hayakuwa sahihi kuwatia hatiani.

Rufaa zilizotupwa ni yenye namba 455/2007 iliyofunguliwa na Kija Nestory akipinga adhabu ya kifo aliyopewa baada ya kutiwa hatiani kwa mauaji ya watu watatu na wizi wa ngombe zaidi ya Hamsini.


Katika Rufaa hiyo Kija alipinga adhabu hiyo huku akidai kwamba  ushahidi uliotolewa dhidi yake  ukiwemo wa utambuzi haukuweza kutosheleza na  kuthibitisha yeye kutiwa hatiani kama ilivyoamuriwa.

Awali katika kesi ya msingi ilidaiwa kwamba tarehe 20 Agosti 1999 katika kijiji cha Mwangali  Mkoani Shinyanga   mrufani  aliwaua Masigana Nundu, Nsamaka Jilala  na Ngwalu Chele.

Jopo la Majaji wa Mahakama ya Rufaa chini ya uenyekiti wa Jaji Nathalia Kimaro, Jaji William Mandia na Jaji Simon Kaijage pia limetupilia mbali rufaa ya Masima Mohamed  aliyetiwa hatiani kwa kosa la ubakaji.

Akisoma maamuzi ya rufaa hizo kwa niaba ya Majaji hao Kaimu Msajili wa Mahakama hiyo Maximillian Malewo, Alisema kuwa  waliosikiliza shauri hilo  lililokuwa na mashitaka mawili  aliyoyatenda 19 Novemba 2003 walithibitisha  makosa   dhidi ya mrufani pasipo shaka yoyote.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa