Home » » Sekondari ya Kata yaanza kutoa wanasayansi

Sekondari ya Kata yaanza kutoa wanasayansi

WAKATI Sekondari Nyingi za Kata Nchini zikiwa hazina majengo ya maabara na kama yapo hayajakamilika,Sekondari ya Kata ya Kazaroho tayari imeanza kutumia majengo yake ya maabara na mwaka huu wanafunzi wake wa kidato cha nne watafanya Mtihani wa  Kitaifa kwa vitendo.

Hatua hiyo inaweka matumaini kwa wanafunzi wa shule hiyo wengi wao sasa kuanza kusoma masomo ya Sayansi na kuamini Shule za Kata zitakuwa mkombozi kwa wanafunzi na jamii kwa ujumla ikiwa zitapewa msaada zaidi.

Akizungumzia hali hiyo,Mkuu wa Shule hiyo,Mwalimu George Ndaki,amesema ana matumaini shule yake itafanya vizuri,akiongeza shule za Kata zisibezwe kwani zina uwezo wa kutoa wataalamu watakaolisaidia Taifa.

Diwani wa Kata ya Kazaroho,Mh Haruna Kasele,amebainisha kuwa tayari wameanza kuona matunda ya sekondari za Kata kwa wanafunzi wake watano kujiunga na Chuo Kikuu mwaka jana huku lengo lao likiwa ni kuinua Elimu kwenye Kata ya Kazaroho.

Diwani Kasele amesema sasa msisitizo utakuwa ni kuwahimiza wanafunzi kusoma masomo ya sayansi kwa vile Maabara na madawa yapo ili wapatikane wanasayansi wa fani mbalimbali watakaolisaidia Taifa

Shule hiyo ya Kazaroho ni mojawapo ya shule tatu za Halmashauri ya wilaya ya Urambo yenye Wilaya mbili za Urambo na Kaliua ambazo majengo yake ya maabara yamekamilika na yanatumika.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa