Home » » PSPF yazawadia wanachuo Chuo cha Ualimu Tabora

PSPF yazawadia wanachuo Chuo cha Ualimu Tabora

MFUKO wa Pesheni kwa watumishi wa umma (PSPF) Mkoani Tabora, umetoa tuzo ya Taaluma  kwa wanachuo watatu wa Chuo cha Ualimu Tabora, waliofanya vyema kwenye mitihani yao kwa mwaka 2012/2013.
Afisa Mfawidhi wa PSPF Peter Rushaki amesema  PSPF imeanzisha huduma mpya ya utoaji tuzo za kitaaluma kwa waalimu watarajiwa, ambazo zitakuwa zikitolewa kwa wanafunzi wa mwaka wa mwisho kwenye vyuo vya ualimu, ambapo chuo cha Ualimu Tabora kimepewa kipaumbele.
Amesema lengo ni kutoa motisha na kuinua kiwango cha elimu kwa walimu watarajiwa waliopo Vyuoni.
Waliozawadiwa kwa kufanya vizuri ni Michael Charles aliyezawadiwa shilingi Laki tatu kwa kuwa mshindi wa kwanza, Ayoub Kibamba,mshindi wa pili alizawadiwa shilingi Laki Mbili na Joyce Kipeta aliyepata shilingi laki moja kwa kuwa mshindi wa tatu.
Akizungumza kwenye halfa hiyo, Mkuu wa Chuo cha Ualimu Tabora, Sister Agnes Awaki, ameishukuru  PSPF kwa hatua waliyofikia na kwamba yeye na wanachuo wana imani kubwa sana na mfuko huo akisema amefurahiswa na hatua hiyo na kwamba kila mara amekuwa akiwasisitiza wanachuo kusoma kwa bidii na angependa kuona wanaweka jitihada zaidi kwenye masomo.
Naye Michael Charles, mwanachuo aliyepata zawadi ya kwanza ya shilingi Laki tatu, akizungumza kwa niaba ya wenzake, ameishukuru PSPF kwa jitihada zao za kuwajali wanachuo   na kwa uamuzi wao wa kuweka tuzo hiyo ya kitaaluma kwa walimu watarajiwa kwani ni hamasa kwa walimu kujiunga na mfuko huo.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa