BAADHI
ya Vyama vya kuweka na kukopa ,SACCOS ,Mkoani Tabora vinakabiliwa kuwa
katika hali mbaya kifedha kutokana na makato ya mikopo ya walimu kutowasilishwa
katika SACCOS hizo.
Katibu
wa chama cha walimu Mkoani Tabora, Bi Romana Alloys,amesema makato ya walimu
hayawasilishwi katika vyama hivyo na kuviweka katika hatari ya kufa.
Akisoma
risala katika uzinduzi wa Jengo la walimu Mkoani Tabora,Katibu huyo amezitaka
halmashauri zote kutoa ushirikiano wa kutosha kwa SACCOS hizo ili ziendelee
kuwahudumia wanachama wao.
Amezitaja
changamoto zinazowakabili walimu kuwa ni nyingi lakini kazitaja baadhi kuwa
Halmashauri nyingi kuchelewesha upandishaji madaraja ya walimu sanjali na Vyeo
Bi
Romana amesema tangu CWT ianze jitihada zake za kuwatetea waalimu
hapa nchini mnamo mwaka 1993, wamepata mafanikio makubwa ikiwemo
kuwaunganisha waalimu wote na kutambuliwa na serikali na kujenga majengo
ya vitega uchumi katika mikoa yote hapa nchini, jitihada ambazo zinaendelea
mpaka sasa.
Jengo
hilo la kitega uchumi lenye Gorofa mbili limejengwa na kampuni ya ujenzi ya
SUMA JKT kwa gharama ya shilingi Milioni 347.
0 comments:
Post a Comment