Home » » Ugonjwa wa kiharusi janga kubwa Tabora

Ugonjwa wa kiharusi janga kubwa Tabora

MKOA wa Tabora una idadi kubwa ya wagonjwa wa Kiharusi ingawa wengi hawajitokezi kupata tiba Hospitalini badala yake wanatibiwa nyumbani.

Mganga mkuu wa Mkoa wa Tabora,Dk.Leslie mhina,amesema kumekuwa na wagonjwa wengi wa kiharusi Mkoani Tabora hali ambayo mwanzoni walidhani tatizo sio kubwa.

Amesema Kiharusi ni tatizo kubwa na hilo wamebaini baada ya kugundua idadi kubwa ya wagonjwa wa kiharusi wanatibiwa kienyeji wakiwa majumbani huku tiba kubwa ikiwa ni kufukuziwa mavi ya tembo.

Amesema wananchi wengi hawaamini kama Kiharusi kinatibiwa hospitalini endapo matibabu yatafanyika mapema na kuwataka wananchi kuwawahisha wagonjwa ili wapate tiba haraka na sio kukimbilia kuwatibu kienyeji.

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa