Home » » 3 wafa kwa kula uyoga wa porini

3 wafa kwa kula uyoga wa porini

Watu watatu wakazi wa Kijiji cha Igunguli, Kata ya Uyogo, Wilaya ya Urambo, mkoani Tabora, wamefariki dunia baada ya kula chakula kinachodhaniwa kuwa na sumu.
Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya hiyo, Dkt. Kheri Kagya, alisema chakula hicho kililiwa na watu wanane ambacho ni ugali na mboga ya uyoga uliochumwa porini ambao ndio unadhaniwa kuwa na sumu.
Waliofariki ni watoto Kija Makoye (3) akiwa njiani kupelekwa Hospitali ya Wilaya hiyo, Wande Mahinge (5) na Mahigi Tongele ambao walikufa wakati wakipatiwa matibabu.
Dkt. Kagya alisema baadhi ya walionusurika katika tukio hilo ni pamoja na mtoto Gimili Makoye (miezi kumi), Talekwa Mahigi (3) na mpishi wa chakula hicho, Nyanzobe Mswahili (25).
 "Tulishindwa kuchukua sampuli ya chakula kinachohisiwa kuwa na sumu kwa sababu kililiwa chote, hata aina ya uyoga tumeshindwa kuutambua kwa vile nao ulichumwa wote.
"Mswahili alitueleza kuwa, uyoga aliochuma porini ulikuwa unafanana na waliowahi kula hivyo hatukuutambua," alisema.
Kamanda wa Polisi mkoani humo, Kamishna Msaidizi wa Polisi Peter Ouma, amethibitisha jeshi hilo kupokea taarifa za tukio hilo

Chanzo;Majira

0 comments:

 
Supported by Tone Multimedia Company Limited : |
Copyright © 2012. Tabora Yetu - All Rights Reserved
Designed by Fredy Tony Njeje
Proudly powered by Blogs za mikoa